IQNA

Tizama Qiraa ya Qur'ani ya kijana Mmisri mwenye uwezo wa kuiga maqarii 11

18:07 - June 02, 2020
Habari ID: 3472828
TEHRAN (IQNA) – Hussein Abdul Zahir ni kijana Mmisri ambaye ana uwezo wa kuiga qiraa ya wasomaji Qur'ani 11 maarufu duniani.

Uwezo wake wa kusoma Qur'ani kwa ustadi uligunduliwa na Sheikhe mmoja wakati akiwa bado katika shule ya msingi.

Alihimizwa sana na Sheikhe huyo kuimarisha kipaji chake cha qiraa ya Qur'ani Tukufu sambamba na kutafakari kuhusu mafundisho ya kitabu hicho kitakatifu.

Klipu ya video iliyohapo chini inmuonyesha Abdul Zahir akiseoma Surah moja ya Qur'ani kwa kuiga maqarii mbali mbali.

Abdul Zahir ana uwezo wa kuiga usomaji wa maqarii maarufu kama Sheikh Muhammad Ayub, Khalil al-Hisri, Mohamed al-Minshawi, Ali Abdullah Jaber, Fares Ibad na Mohamed Jibril.

3902662

Kishikizo: qiraa qurani tukufu
captcha