Kituo cha Kiislamu cha Malawi kiliandaa mjumuiko huo, ambao ulihudhuriwa na wanafunzi wa tawi la Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa nchini humo.
Wanafunzi hao walibeba mabango na kutoa nara za kulaani jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel hasa mauaji ya watoto huko Palestina.
Malawi ni nchi isiyo na bandari kusini mashariki mwa Afrika. Takriban asilimia 25 ya wakazi nchini humo ni Waislamu ambao aghalabu wanaishi katika Kanda ya Kusini.
Utawala wa haramu wa Israel umekuwa ukiushambulia Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya wiki tatu, baada ya operesheni ya kushtukiza iliyoanzishwa na Hamas kwa lengo la kujibu jinai za utawala huo katili.
Mashambulizi hayo ya Israel hadi sasa yamepelekea takriban Wapalestina 9,000 kupoteza maisha tokea Oktoba 7 ambapo wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto.
3485853