Ripoti hiyo inaangazia matukio ambapo Waislamu hupata shida kupata miadi ya matibabu na wanakabiliwa na ubaguzi.
Hasa, ripoti hiyo inaangazia matukio ambapo wafanyikazi wa matibabu wanadaiwa kuwabagua na kuwadharau wagonjwa Waislamu, haswa wanawake.
Asili ya ubaguzi huu ni hali ya kisiasa ya harakati za mrengo wa kulia wenye misimamo mikali kote Ulaya. Uchaguzi wa hivi majuzi wa Bunge la Ulaya uliashiria mabadiliko ndani ya kambi hiyo yenye wanachama 27, huku vyama vyenye mrengo wa kulia vinavyoeneza chuki dhidi ya Waislamu vikipata viti zaidi.
Nchini Ujerumani, chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha Mbadala kwa Ujerumani (AfD) kilipanda hadi nafasi ya pili, na kunyakua takriban asilimia 16 ya kura. Wakati huo huo, huko Ufaransa, mrengo wa kulia umepata umashuhuri kiasi kwamba Rais Emmanuel Macron alivunja bunge la kitaifa na akaitisha uchaguzi wa haraka. Chama cha mrengo wa kulia kimepata thuluthi moja ya viti 31, zaidi ya mara mbili ya uungwaji mkono wa chama cha Macron.
Ripoti ya ECRI pia inaangazia maamuzi ya sera ambayo yanazidisha ubaguzi kama vile marufuku ya Ufaransa kwa wasichana wa shule kuvaa vazi la kiislamu la Hijabu. Vile vile, jimbo la Baden-Wuerttemberg nchini Ujerumani limepiga marufuku Hijabu kwa watoto wote wa shule.
Wakati huo huo, matukio ya chuki yameongezeka kufuatia kuanza kwa vita vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapales Gaza mnamo Oktoba 7.
ECRI imebainisha wasiwasi wake mkubwa kuhusu kuongezeka kwa chuki na ubaguzi dhidi ya Waislamu barani Ulaya. Tume hiyo inatoa wito kwa nchi wanachama wa Baraza la Ulaya kutekeleza kikamilifu sera zake ili kukabiliana na mienendo hii inayosumbua.
3488836