IQNA

Msaada

Madaktari 7,000 wa Iran wajitolea kuelekea Lebanon huku Israel ikiendeleza vita

19:03 - October 07, 2024
Habari ID: 3479552
IQNA - Idadi kubwa ya wataalam wa matibabu wa Iran wametoa wametangaza utayari wao wa kwenda Lebanon kuwahudumia watu wa nchi hiyo ya Kiarabu huku utawala wa Kizayuni, ukiendeleza vita dhidi ya nchi hiyo, afisa mmoja alisema.

Madaktari 7,000 wa Iran wajitolea kuelekea Lebanon huku Israel ikiendeleza vitaPir Hossein Koulivand, Mkuu wa Jumuiya ya Hilali Nyekundu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, zaidi ya matabibu na wataalamu 7,000 wa fani tofauti za matibabu wamejitolea kutumwa Lebanon.

Wako tayari kwenda katika nchi hiyo ya Kiarabu na kujiunga na juhudi za kuwasaidia watu waliokumbwa na vita huko, alisema.

Koulivand pia amebainisha kuwa katika kipindi cha siku kumi zilizopita, wananchi wa Iran wamechangisha rial bilioni 40 kupitia Jumuiya ya Hilali Nyekundu ya Iran ili kuwasaidia watu wa Ukanda wa Gaza, Yemen na Lebanon.

Wimbi la mashambulizi ya anga ya Israel katika maeneo makubwa ya Lebanon yameua maelefu ya watu wakiwemo wanawake na watoto katika kipindi cha wiki chache zilizopita.

Watu wengi pia wamelazimika kuyahama makazi yao kutokana na hujuma za utawala ghasibu wa Israel.

4240921

captcha