gaza

IQNA

IQNA – Katikati ya maangamizi yaliyosababishwa na vita vya mauaji ya kimbari vilivyotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza, Shule ya Qur'ani ya Noor iliyopo Khan Yunis inaendelea kujitahidi kufungua dirisha jipya la maisha.
Habari ID: 3482283    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/25

IQNA – Watetezi wa haki za binadamu na maafisa wa Palestina wameilaani hatua wanayoieleza kuwa ni kukiuka kwa mfumo uhuru wa ibada, baada ya utawala haramu wa Israel kwa mara nyingine kuzuia maelfu ya Wapalestina wa Gaza kusafiri kwenda Saudi Arabia kwa ajili ya Hija ya kila mwaka.
Habari ID: 3482268    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22

IQNA – Katika programu iliyofanyika Gaza, watoto 65 walioshiriki katika kampeni ya Qur’ani ya “Nuur” walisoma sehemu za Qur’ani Tukufu mbele ya walimu wao, kisha wakatunukiwa na kupongezwa na viongozi pamoja na wazazi wao.
Habari ID: 3482263    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/20

IQNA – Mufti Mkuu wa Oman ametoa wito kwa Waislamu kusimama kwa umoja katika kukabiliana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi za Kiislamu.
Habari ID: 3482224    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/10

IQNA – Kwa zaidi ya miaka miwili sasa, vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendeshwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vimegeuza mitaa mizima ya mji wa Gaza kuwa magofu ya simenti na vyuma vilivyopinda.
Habari ID: 3482219    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/09

IQNA – Utawala wa Israel unakabiliwa na ukosoaji wa pamoja usio wa kawaida kutoka Hispania na Brazil baada ya jeshi lake la wanamaji kuwakamata raia wawili wa nchi hizo kutoka katika meli iliyokuwa ikielekea Gaza katika maji ya kimataifa, kitendo ambacho serikali zote mbili zimesema ni kinyume cha wazi cha sheria za kimataifa.
Habari ID: 3482192    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/02

IQNA – Waandaaji wa msafara mkubwa wa kibinadamu wa meli unaoelekea Gaza wamesema kuwa vikosi vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimejaribu kuuzuia msafara huo, kwa kuzuia baadhi ya meli katika maji ya kimataifa kwa kutumia ndege zisizo na rubani (drones), kuvuruga mawasiliano na askari waliopanda meli kwa nguvu.
Habari ID: 3482184    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/30

IQNA – Kwa zaidi ya miaka 50, Chama cha Leba kimekuwa kikichukulia Newham, Uingereza kama ngome yake salama ya kisiasa.
Habari ID: 3482170    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/27

IQNA – Kwa karne nyingi, Msikiti Mkuu wa Omari umesimama kama mlinzi kimya wa historia ya kielimu ya Gaza, hukoo Palestina huku maktaba yake ikihifadhi maandiko ya kale yaliyoandika simulizi za kupanda na kushuka kwa ustaarabu mbalimbali.
Habari ID: 3481992    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/25

IQNA-Jua lilipotua juu ya Gaza siku ya Jumanne, safu za waumini zilisimama kuswali, si ndani ya misikiti, bali juu ya magofu yake.
Habari ID: 3481957    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/19

IQNA-Maelfu kwa maelfu ya watu wamejitokeza mitaani katika nchi kadhaa za Ulaya kushiriki maandamano ya kuunga mkono Palestina, huku wakiushutumu utawala dhalimu wa Israel kwa kukiuka mara kwa mara makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza kati yake na Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas.
Habari ID: 3481878    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/01

IQNA –Afrika Kusini imemtan gaza kaimu balozi wa utawala wa Isarel nchini humo kuwa mtu asiyehitajika na kuamuru afukuzwe mara moja.
Habari ID: 3481876    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/31

IQNA-Ripoti ya pamoja ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu ya Palestina imeripoti kuwa, kuanzia Oktoba 2023 hadi Oktoba 2025, walimu wasipungua 1,377 na wafanyakazi wa elimu waliuawa shahidi na 4,757 wamejeruhiwa katika mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala dhalimu wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3481824    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/20

IQNA: Baada ya kufariki kwa idadi ya watoto wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza kutokana na baridi kali, Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombzoi wa Palestina, Hamas, imeonya kuhusu kuzidi kuzorota kwa hali ya kibinadamu katika eneo hilo ambalo liko chini ya mzingiro wa utawala katili wa Israel.
Habari ID: 3481801    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/14

IQNA – Tangu kuanza kwa vita vya kikatili vinavyoendeshwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza, angalau Wapalestina 21 wamefariki katika eneo hilo kutokana na baridi kali na ukosefu wa vifaa vya kujihifadhi na kupashia joto, hali ambayo imesababisha na hatua ya Israel kuzuia misaada kufika eneo hilo.
Habari ID: 3481797    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/13

IQNA-Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amezinukuu ripoti za kiitelijinsia na kusema kuwa eneo lililojitenga la na nchi hiyo la Somaliland limekubali kuwapokea Wapalestina na kuanzishwa kambi ya kijeshi ya Israel katika eneo hilo mkabala wa kutambuliwa rasmi na Israel.
Habari ID: 3481750    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/01

IQNA- Utawala haramu wa Israel unaendelea kulaaniwa vikali  baada ya kushambulia kikatili sherehe ya harusi Gaza huku shirika mashuhuri la haki za kiraia za Waislamu nchini Marekani likitaka jumuiya ya kimataifa kuingilia kati.
Habari ID: 3481694    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/21

IQNA – Shule mpya ya Qur’ani imefunguliwa mjini Gaza kwa mchango wa kampeni ya wananchi wa Iran inayojulikana kama “Iran Hamdel” kwa ushirikiano na Taasisi ya Ahl al‑Quran ya Gaza.
Habari ID: 3481675    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/17

IQNA – Watoto arobaini na wanne wa mashahidi ambao wamehifadhi Qur’ani Tukufu wameheshimiwa katika hafla maalumu huko Gaza.
Habari ID: 3481661    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/15

IQNA – Mkuu wa Shirika la Utan gaza ji la Umma nchini Uhispania (RTVE), José Pablo López, amemkemea Mkurugenzi wa Mashindano ya Muziki ya Eurovision kwa barua yake ya wazi kwa mashabiki ambayo haikutaja Gaza wala utawala wa Israel, akisema hatua hiyo ni “kushindwa” wakati mashindano hayo yanapitia mgogoro mkubwa wa kiheshima.
Habari ID: 3481653    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/13