IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeendesha oparesheni kubwa ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya vituo nane vya kijeshi vya Marekani katika kanda hii, likiitaja hatua hiyo kuwa “jibu madhubuti” dhidi ya uchokozi mpya wa Marekani kwenye ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482414 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28
IQNA-Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Mkataba wa Maelewano (MoU) wa kumaliza vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa matokeo ya shinikizo au kulazimishwa, bali ni zao la ustahimilivu na nguvu ya taifa shupavu la Iran.
Habari ID: 3482399 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24
IQNA-Rais wa Iran ametoa wito wa ushirikiano wa karibu zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu, akisema Iran imenyoosha “mkono wa urafiki” kwa nchi za kanda hii katika harakati za kutafuta mfumo mpya wa usalama.
Habari ID: 3482398 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24
IQNA – Maombolezo ya Muharram kwa ajili ya Imam Hussein (AS) yamefanyika karibu na Husseiniyeh ya Imam Khomeini (RA) jijini Tehran, siku ya Jumapili jioni.
Habari ID: 3482391 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/22
IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, amesema maafisa wa Iran wamefanya juhudi kubwa kwa nia njema na kwa kujali maslahi ya taifa ili kufikia hati ya makubaliano (MoU) na Marekani, huku rais wa Marekani akitumia mbinu mbalimbali kutokana na hali ya kukata tamaa.
Habari ID: 3482379 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/19
IQNA-Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani sasa imetiwa saini rasmi na marais wa nchi hizo mbili baada ya maandishi yake kukamilishwa, na hivyo makubaliano hayo kuanza kutekelezwa. Hayo yametangazwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Jumatano usiku.
Habari ID: 3482374 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/18
IQNA – Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani imepongezwa na Papa Leo XIV, ambaye ameielezea kuwa hatua muhimu ya kujiepusha na vita.
Habari ID: 3482371 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/17
IQNA-Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
Habari ID: 3482361 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/15
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
Habari ID: 3482349 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/11
IQNA – Katika kauli yenye ukali dhidi ya sera za Rais wa Marekani Donald Trump, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesema kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran havina uhalali wa maadili.
Habari ID: 3482334 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeshambulia kambi mbili za anga za Marekani huko Kuwait na vituo vilivyobaki vya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani (US Fifth Fleet) huko Bahrain ili kujibu uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani.
Habari ID: 3482327 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06
IQNA – Mstahiki Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, amelaani vikali vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran akivitaja kuwa ni mgogoro usio na msingi, na kusisitiza kuwa vita hivyo ni lazima viishe mara moja kwa ajili ya usalama wa raia wa mataifa mengine, na pia kwa manufaa ya Wamarekani wanaopambana na hali ngumu ya maisha nyumbani kwao.
Habari ID: 3482297 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/29
IQNA – Rais wa Iran Masoud Pezeshkian katika ujumbe wake kwa Papa Leo XIV ameshukuru misimamo ya kimaadili ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki kuhusu mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, akiyataja kuwa ni ukiukaji wa utawala wa sheria na wa maadili ya kibinadamu.
Habari ID: 3482246 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16
Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa
IQNA-Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa kimesema kuwa ushiriki, uwezeshaji na ushirikiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika vita vya hivi karibuni vya uchokozi vilivyoanzishwa na Marekani pamoja na utawala wa Israel dhidi ya Iran ni sawa na “kusaidia kambi ya ukafiri dhidi ya ndugu Waislamu” na kwa hivyo ni “haramu kabisa.”
Habari ID: 3482238 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/14
IQNA – Papa Leo XIV amemtunuku Hujjatul‑Islam Mohammad Hossein Mokhtari, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Vatican, nishani ya juu zaidi ya kidiplomasia ya Vatican.
Habari ID: 3482235 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13
IQNA – Kwa zaidi ya miaka miwili sasa, vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendeshwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vimegeuza mitaa mizima ya mji wa Gaza kuwa magofu ya simenti na vyuma vilivyopinda.
Habari ID: 3482219 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/09
Rais wa Iran katika Mazungumzo ya Simu na Rais wa Ufaransa:
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemwambia mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuwa Tehran iko tayari kuendelea kwa dhati kupitia njia za kidiplomasia ili kukomesha vita, huku ikisisitiza umuhimu wa kulindwa kwa haki za taifa la Iran.
Habari ID: 3482213 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/07
IQNA – Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitaka serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kusitisha kujipanga upande mmoja na kushirikiana na pande zinazoiwekea uadui Jamhuri ya Kiislamu.
Habari ID: 3482210 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/07
IQNA-Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu imetangaza Jumapili kuwa Gaza imegeuka kuwa sehemu hatari kuliko zote duniani kwa wanahabari, huku angalau wafanyakazi 295 wa vyombo vya habari wakithibitishwa kuuawa katika mashambulizi ya Israel tangu kuanza kwa vita Oktoba 2023.
Habari ID: 3482200 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/04
IQNA – Mtaalamu wa Qur’ani Tukufu kutoka Lebanon amekosoa misimamo ya qari mmoja kutoka Kuwait akisema kuwa haina uhusiano na mafundisho ya Qur’ani.
Habari ID: 3482177 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29