IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Kuwait Yazindua Mashindano ya 13 ya Kimataifa ya Qur'ani

20:24 - November 15, 2024
Habari ID: 3479752
IQNA - Sherehe za uzinduzi wa mashindano ya 13 ya kimataifa ya Qur'ani ya Kuwait zilifanyika katika mji wa Kuwait Jumatano jioni. Waziri wa Masuala ya Kiislamu na Wakfu Mohammad Al-Wasmi, wajumbe wa jopo la majaji na washindani walihudhuria sherehe za ufunguzi.

Waziri wa Al Wasmmmmi alisema katika hotuba yake kwamba, watu wa Kuwait wamejitahidi kuitumikia Qur'ani na kuhifadhi na kuzifanyia kazi aya za Mwenyezi Mungu kwa vizazi vingi.
Mzungumzaji mwingine alikuwa Naibu Waziri wa Wafu Badr al-Matiri ambaye aliangazia maendeleo ya shindano hilo katika suala la ubora na wingi kwa miaka mingi.
Alisema washiriki 127 kutoka nchi 75 wanashiriki katika toleo hili la shindano hilo.
Tuzo ya 13 ya Kimataifa ya Qur'ani ya Kuwait, inayoshirikisha mashindano ya kuhifadhi Qur'ani, usomaji na Tajweed, itaendelea hadi tarehe 20 Novemba.
Iran ina wawakilishi watatu katika tukio la Qur'ani.
Habib Sedaqat anashindana katika kategoria ya usomaji wa Qur’ani naye Mohammad Reza Zahedi anawania tuzo ya juu katika kitengo cha kuhifadhi Qur’ani kwa watu wazima.
Mwakilishi wa Iran katika kuhifadhi Quran nzima kwa ajili ya watoto ni Mohammad Hossein Malekinejad.
Tangu kuanzishwa kwake mwaka wa 2010, mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya Kuwait, yanayoandaliwa na Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu ya Kuwait, yanalenga kuwahimiza vijana duniani kote kujihusisha na Qur'ani kwa kuhifadhi na kuisoma.
Mwaka huu; kategoria kadhaa ambazo kuhifadhi Qur'ani nzima, qiraa kwa mitindo kumi ya usomaji,  kuhifadhi kwa vijana, na kategoria maalum ya mradi bora wa kiufundi unaohudumia Qur’ani.
Kuna majaji na washiriki kutoka nchi  85 ambapo miongoni mwa washindani 127, 75 watashiriki katika kategoria ya kuhifadhi, 16 katika kategoria ya mitindo kumi ya qiraa, 13 katika qiraa na 23 katika kategoria ya kuhiadhi kwa vijana.
Maonyesho yenye mada "Kama Ulivyojifunza" yataendeshwa sambamba na shindano hilo. Maonyesho hayo yataonyesha mbinu mbalimbali za kuhifadhi, mitindo ya qiraa ya Qur'ani, na maendeleo katika mbinu za kuhifadhi, na kuwapa waliohudhuria ufahamu wa urithi wa elimu na utamaduni wa Qur'ani.

3490687

captcha