Kozi hii ya kwanza ya kiangazi imeandaliwa na Kituo cha Elimu ya Qur'ani cha Al Noor, ambacho kipo chini ya Idara ya Da’wa na Mwongozo wa Kidini katika Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Qatar.
Mpango huu wa wiki tatu ulibuniwa kuwasaidia wanafunzi kuimarisha uhifadhi wao wa Qur'ani Tukufu sambamba na kukuza uwezo wao wa kielimu na kitaaluma wakati wa mapumziko ya kiangazi, kwa mujibu wa ripoti ya Qatar Tribune iliyotolewa Jumatano.
Kama sehemu ya ratiba, kila mwanafunzi alitarajiwa kuhifadhi kurasa mbili za Qur’ani kila siku pamoja na kupitia sehemu walizokwisha zihifadhi hapo awali.
Kozi hii ni sehemu ya mfumo mpana wa elimu unaojumuisha masomo ya misingi ya Qur’ani, ibada za vitendo, mafunzo ya sauti (makhraj na tajweed), shughuli za mwili, na matembezi ya elimu na burudani.
Mbali na masomo ya dini, wanafunzi walihudhuria pia vipindi vya taaluma mbalimbali kama vile usalama wa mitandao (cybersecurity). Aidha, programu ilihusisha warsha za kaswida (chanting) na mafunzo ya kutoa Adhana (mwito wa swala).
3493972