Mus’haf ni neno la Kiarabu la kodeksi au mkusanyiko wa karatasi, lakini pia humaanisha’ nakala iliyoandikwa ya Qur’ani.
Al-Ubaidi aliandika kaligrafia ya Mus’haf wa Qatar, ambao ulichapishwa mwaka 2010. Hadi sasa zaidi ya nakala 700,000 za Mus’haf huo zimechapishwa.
Aliiambia Al Jazeera kwamba kaligrafia ya Mus’haf ni ndoto ya kila Mwislamu mwandishi wa kaligrafia na kwamba anafurahi sana Mwenyezi Mungu amemuwezesha kutimiza ndoto yake.
Ili kuandika aya za Qur'an, mwandishi wa kaligrafia anapaswa kuitakasa nafsi yake kutokana na majivuno, kiburi, na mengine kama hayo, alisema.
Al-Ubaidi alichaguliwa kwa kazi hiyo baada ya kuhudhuria shindano la kimataifa la uandishi wa Kaligrafia.
Tukio hilo lililofanyika mwaka wa 2001 lilivutia takriban watu 120 waliobobea katika ulimwengu wa Kiislamu ambao walishindana hawakuweza kuidhinishwa na jopo la kimataifa la wataalamu wa sanaa ya uandishi wa Kiarabu.
Baada ya jopo la wataalamu Oktoba 2002 huko Istanbul lilitangaza kwamba shindano hilo lilikuwa na wanakaligrafia wawili pekee watakaowania kuandika Mus’haf wa Qatar; Mikataba ya uandishi ilitiwa saini huko Doha mnamo Juni 2003, ili kuanza hafla mchakatano wa kuandika nakala maalumu ya Qur’ani Tukufu ya Qatar.
Mnamo Januari 2007, jopo hilo lilitangaza kuwa al-Banki ameteuliwa kuwa mwandishi rasmi wa Mus’haf wa Qatar.
Al-Banki alitumia miaka 2.5 kuandika Mus’haf wa Qatar, ambao baadaye ulipelekwa Misri kwa ajili ya kusahihishwa na kisha kupelekwa Istanbul, Uturuki kwa uchapishaji.
3488362