IQNA

Washindi wa Mashindano ya Qur'ani kwa Watoto Doha wapata zawadi

16:14 - March 22, 2025
Habari ID: 3480416
IQNA – Watoto wadogo waliochukua walioshika nafasi za juu katika toleo la 30 la Mashindano ya Qur'ani ya Sheikh Jassim bin Mohammed bin Thani nchini Qatar wameitunukiwa tuzo.

Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya nchi hiyo iliwatunuki washindi Ijumaa.

Jumla ya Waqatari 604 (wanaume na wanawake) na wakaazi 1,482 (wanaume na wanawake) walipokea zawadi za kifedha na vyeti katika sherehe iliyofanyika katika Msikiti wa Imam Muhammad bin Abdul Wahhab katika mji mkuu, Doha.

Zaidi ya watoto 3,000 walishiriki katika kipengele  na kufanya toleo la mwaka huu kuwa na ushindani zaidi kuliko mwaka mwingine wowote.

Kulingana na sheria za tawi hili, raia wenye umri wa miaka 12 au chini na wakaazi wenye umri wa miaka nane au chini wanashiriki katika moja ya Juzuu tano za mwisho za Qur'ani Tukufu.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kuandaa Jassim Abdullah Al Ali alisisitiza umuhimu wa Awqaf katika kuwaheshimu na kuwaenzi wanaohifadhi au kusoma Qur'ani, ili kuwahamasisha waendelee kufuata na kuendeleza amali hiyo njema.

3492464

Habari zinazohusiana
Kishikizo: qatar qurani tukufu
captcha