IQNA

Kongamano la Kimataifa la “Utalii na Masuala ya Kiroho” kufanyika Tehran

20:41 - May 16, 2026
Habari ID: 3482244
IQNA – Kongamano la Tano la Kimataifa kuhusu Utalii na Masuala ya Kiroholinatarajiwa kufanyika mjini Tehran siku ya Jumatano, tarehe 20 Mei.

Kongamano hilo litaandaliwa na Chuo Kikuu cha Sayansi na Utamaduni, likifanyika kwa njia ya kuhudhuria moja kwa moja pamoja na mtandaoni.

Tukio hili la kitaalamu linalenga kuboresha ubora wa kongamano na kunufaika na uwezo wa kitaaluma wa wadau mbalimbali wanaovutiwa na mada hiyo. Aidha, litaendeleza mafanikio ya makongamano yaliyopita na kuchunguza uhusiano uliopo kati ya utalii na vipengele vya kiroho katika maisha ya mwanadamu.

Miongoni mwa malengo makuu ya toleo hili ni kuwasilisha matokeo mapya ya tafiti, kupendekeza mitazamo mipya, na kuchunguza nafasi ya utalii wa kiroho katika kuboresha ubora wa maisha ya mtu binafsi na jamii kwa ujumla.

Kutilia mkazo uwezo wa kitamaduni na wa kiroho ndani ya sekta ya utalii , hasa kwa kuzingatia hali ya sasa ya nchi,  ni miongoni mwa masuala muhimu yatakayojadiliwa katika kongamano hili la kimataifa.

Wanaotaka kushiriki kongamano hilo kwa njia ya mtandaoni wanaweza kutembelea:

live.usc.ac.ir/research

Kwa maelezo zaidi, tembelea tovuti ya kongamano:

icts.usc.ac.ir.

3497466

Kishikizo: utalii waislamu uislamu
captcha