TEHRAN (IQNA)- Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeutahadharisha utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kufanya chokochoko na mashambulizi ya aina yoyote dhidi ya mji wa Quds (Jerusalem) na Msikiti Mtukufu wa al Aqsa mjini humo.
                Habari ID: 3473942               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/05/24
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran Ayatullah Ali Khamenei amejibu barua za viongozi wa harakati za mapambano ya kukomboa Palestina za Hamas na Jihad Islami akisisitiza kuwa: Nyoyo zetu ziko pamoja nanyi katika uwanja wa mapambano yenu, na hatimaye mtapata ushindi.
                Habari ID: 3473941               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/05/24
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Harakati ya Mapambano ya Kiislamu Palestina (Hamas) imetangaza ushindi katika mapambano ya siku 10 dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel ambao umevamia Ukanda wa Ghaza na kuongeza kwamba waziri mkuu wa utawala huo Benjamni Netanyahu ameshindwa vibaya katika makabiliano hayo.
                Habari ID: 3473928               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/05/20
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Mkuu wa Idara ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameutaka Umma wa Kiislamu na Kiarabu kufanya maandamano na mikutano ya kutetea na kuunga mkono Msikiti wa al Aqsa na watu wa Palestina.
                Habari ID: 3473908               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/05/14
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amemwandikia barua Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kumjulisha matukio na mabadiliko yanayojiri katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu.
                Habari ID: 3473894               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/05/10
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Kadhia ya wafungwa Wapalestina wanaoshikiliwa katika magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel ni kipaumbele kwa watu wa Palestina.
                Habari ID: 3473830               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/04/19
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) - Harakati za kupigania ukombozi wa Palestina za Fat'h na Hamas zimeunga mkono tangazo la Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuhusu kufanyika uchaguzi wa bunge la rais baadaye mwaka huu.
                Habari ID: 3473561               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/01/16
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Kiongozi mwandamizi Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amewaomba baadhi ya viongozi wa nchi ikiwemo Iran kuunga mkono juhudi zilizofanyika kwa ajili ya kuimaisha umoja na mshikamano wa kitaifa wa Palestina.
                Habari ID: 3473544               Tarehe ya kuchapishwa            : 2021/01/10
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) -Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, sera za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE)  za kuunga utawala wa Kizayuni wa Israel ni kwa madhara ya haki za Wapalestina.
                Habari ID: 3473477               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/12/21
            
                        
        
        Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas), imelaani vikali kitendo cha utawala haramu wa Israel kumuua shahidi kijana Mpalestina aliyekuwa na umri wa miaka 14.
                Habari ID: 3473427               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/12/06
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetuma salamu za rambi rambi kufuatia kuaga dunia waziri mkuu wa zamani wa Sudan Sadiq al-Mahdi na kumtaja kuwa muungaji mkono mkubwa wa Palestina aliyepinga uanzishwaji uhusiano wowote na utawala wa Kizayuni wa Israel.
                Habari ID: 3473399               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/11/27
            
                        
        
        Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amemtaka rais mteula wa Marekani Joe Biden aufutilie mbali mpango wa Marekani-Wazayuni wa Muamala wa Karne, uliojaa njama na hila kwa madhara ya Wapalestina.
                Habari ID: 3473341               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/11/08
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)-  Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema hatua ya baadhi ya nchi za Kiarabu kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel imeupa utawala huo kiburi na ujuba wa kuendelea kupora ardhi za Wapalestina na kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni kinyume cha sheria.
                Habari ID: 3473268               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/10/17
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA)- Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imepinga madai ya afisa mwandamizi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuwa eti utawala bandia wa Israel umesitisha upanuzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni baada ya utawala huo kuanzisha uhusiano na nchi mbili za Kiarabu za UAE na Bahrain.
                Habari ID: 3473222               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/10/02
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeupa utawala haramu wa Israel muhula mwa miezi miwili kuhitimisha mzingiro wake wa miaka 12 dhidi ya Ukanda wa Ghaza.
                Habari ID: 3473194               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/09/22
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) - Ismail HaniYa, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ameonana ana kwa ana na Sayyid Hassan Nasrallah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon na kuzungumza naye mambo muhimu yanayohusiana na kambi ya muqawama.
                Habari ID: 3473144               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/09/07
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) – Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) Ismail Haniya, amefika nchini Lebanon kwa mara ya kwanza baada ya miaka 27.
                Habari ID: 3473130               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/09/02
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) - Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kumtia tena mbaroni kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Palestina ina lengo la kuwafutilia mbali walinzi wa Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem).
                Habari ID: 3473077               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/08/17
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imetoa wito wa kuanzishwa kamati ya mirengo yote ya Palestina kwa ajili ya kuutetea mji wa Quds Tukufu (Jerusalem) na kuulinda kutokana na hujuma ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
                Habari ID: 3473042               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/08/07
            
                        
        
        TEHRAN (IQNA) - Msemaji wa Harakati ya Muqawama ya Palestina (Hamas) amesema kuwa, utawala wa Kizayuni unatekeleza mashambulizi katika Ukanda wa Ghaza lengo likiwa ni kuwahamishia wananchi wa Palestina migogoro ya ndani ya utawala huo na kupotosha fikra za walimwengu kuhusu matukio na hali mbaya ya kisiasa inayoukabili sasa utawala wa Israel.
                Habari ID: 3473028               Tarehe ya kuchapishwa            : 2020/08/03