iqna

IQNA

hamas
Jinai za Israel
IQNA-Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina, Hamas, amethibitisha habari ya kuuawa shahidi watoto na wajukuu zake katika shambulio la kinyama la utawala wa Kizayuni na akasema: "kwa machungu haya na kwa damu hii tunajenga matumaini, mustakbali na uhuru wa watu wetu, piganio letu na taifa letu".
Habari ID: 3478669    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/04/11

Kadhia ya Palestina
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema vikosi vya mapambano ya Kiislamu ya wapigania ukombozi au Muqawama na Wapalestina wote katika Ukanda wa Gaza ndio washindi kwenye medani ya vita na utawala wa Kizayuni wa Israel ni mwangamizaji wa kizazi na akasisitiza kwa kusema: kilele cha kuheshimika na kusimama imara watu wa Gaza na Palestina na kushindwa utawala wa Kizayuni katika vita hivyo vya miezi sita ni tukio na jambo lenye rehma za Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3478598    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/29

Diplomasia ya Kiislamu
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, Muqawama (mapambano ya Kiislamu) usio na kifani wa vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza umeutukuza Uislamu.
Habari ID: 3478588    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/27

Jinai za Wazayuni
IQNA - Lawama zimeongezeka baada ya utawala ghasibu wa Israel kuweka vizuizi katika milango mitatu ya kuelekea Msikiti wa Al-Aqsa katika eneo la Quds (Jerusalem) Mashariki linalokaliwa kwa mabavu.
Habari ID: 3478516    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/15

Jinai za Israel
IQNA - Waziri wa utawala wa Kizayuni mwenye misimamo mikali ya chuki amesema mwezi mtukufu wa Ramadhani unapaswa 'kufutwa' ili kuepusha taharuki katika mji mtakatifu wa al-Quds (Jerusalem).
Habari ID: 3478440    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/03/02

Jinai za Israel
IQNA - Kutakuwa na mlipuko na maafa makubwa hivi karibuni ikiwa utawala wa Kizayuni utaendelea na mpango wa kuwazuia Waislamu kuswali katika Msikiti wa Al-Aqsa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ilionya.
Habari ID: 3478412    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/02/25

Watetezi wa Palestina
IQNA-Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amesema utawala haramu wa Israel umeshindwa kufikia malengo yake yoyote baada ya takriban siku 100 za vita vya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478183    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11

Jinai ya Israel
IQNA-Naibu mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Palestina Hamas ameuawa katika shambulio la kigaidi la ndege isiyo na rubani ya utawala katili wa Israel katika kitongoji cha kusini mwa mji mkuu wa Lebanon wa Beirut.
Habari ID: 3478137    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/03

Mapambano ya Wapalestina
IQNA - Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (Muqawama) ya Palestina, Hamas, Ismail Haniya amesisitiza uthabiti na azma la harakati hiyo katika kuendeleza mapambano ya kupigania ukombozi wa Palestina.
Habari ID: 3478066    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/20

Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA) - Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema watu wa Palestina wataibuka katika vita dhidi ya Gaza wakiwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali.
Habari ID: 3477980    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/03

Jinai za Israel
TEHRAN (IQNA)- Kuanzia jana subuhi Ijuumaa, na mara baada ya kumalizika muda wa kusimamisha vita, utawala wa Kizayuni umeendeleza mauaji ya kikatili kupindukia dhidi ya wananchi wa Ghaza huko Palestina wanaoendelea kuzingirwa kila upande.
Habari ID: 3477972    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/02

Watetezi wa Palestina
TUNIS (IQNA) - Rached Ghannouchi, mkuu wa Chama cha Ennahda cha Tunisia, alielezea Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa kama zawadi kwa Umma wa Kiislamu.
Habari ID: 3477934    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/23

Harakati za Mapambano ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Hizbullah jana Jumatano alikutana na ujumbe wa maafisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS mjini Beirut kujadili matukio ya Gaza, huku idadi ya wananchi wa Palestina waliouawa shahidi kwenye mashambulizi ya kikatili ya Israel katika eneo hilo linalokaliwa kwa mabavu ikikaribia 15,000.
Habari ID: 3477931    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/23

Kimbunga cha Al Aqsa
Israel WASHINGTON, DC (IQNA) - Asilimia 60 ya Waislamu nchini Marekani wanaunga mkono Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa ya Harakati ya Kiislamu ya Kupigania Ukombozi wa Palestina, Hamas, dhidi ya utawala wa Israel, wakisema kundi hilo la kupigania ukombozi lilikuwa na haki katika mashambulizi yake.
Habari ID: 3477896    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/15

Kadhia ya Palestina
TEHRAN (IQNA)- Mkuu wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) na ujumbe alioandamana nao wamekutana na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Khamenei.
Habari ID: 3477847    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/06

Kimbunga cha Al Aqsa
TEHRAN (IQNA)- Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ameilaani vikali Marekani kutokana na uungaji mkono wake usio na masharti kwa kampeni ya kijeshi ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Ghaza. Aidha amesema utawala wa Israel umepata idhini ya Marekani ya kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3477842    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/11/05

AL-QUDS (IQNA) - Shambulio la anga la Israel limepiga  msikiti mmoja huko Jenin, eneo linalokaliwa kwa mabavu la Ukingo wa Magharibi, huku kukiwa na mashambulizi ya mabomu katika Ukanda wa Gaza ambayo yamegharimu maisha ya zaidi ya Wapalestina 4,300. 
Habari ID: 3477776    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/10/23

TEHRAN (IQNA) - Mashambulizi ya usiku ya wanajeshi wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza yamegharimu maisha ya watu 46 licha ya Hamas kuwachilia mateka wawili wa Kimarekani siku ya Ijumaa.
Habari ID: 3477773    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/10/22

Ukombozi wa Palestina
TEHRAN (IQNA) Harakati ya Mapambano (Muqawama) ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imekosoa vikali kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ya kuyataka mapambano ya wapigania ukombozi Wapalestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel kuwa eti ni "vurugu" na kusisitiza kwamba kinachofanyika katika ardhi za Palestina ni haki ya kujihami dhidi ya utawala unaokalia ardhi kwa mabavu.
Habari ID: 3477602    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/09/15

Mapambano ya Kiislamu (Al-Muqawama Al-Islamiya)
TEHRAN (IQNA)- Viongozi wa harakati za mapambano ya Kiislamu (Al-Muqawama Al-Islamiya) za Palestina na Lebanon wameapa kushirikiana ili kutoa jibu la pamoja dhidi ya sera za uvamizi za utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3477543    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/09/03