palestina - Ukurasa 53

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Mkutano wa pili wa kimataifa wa Umoja wa Maulamaa wa Muqawama au mapambano ulianza hapo jana Jumatano katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut kwa kaulimbiu ya "Umoja kwa ajili ya Palestina-Israel inaelekea kutoweka".
Habari ID: 3471244   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/11/02

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma ujumbe katika Mkutano wa Pili Muungano wa Kimataifa wa Maulama wa Muqawama unaofanyika huko Lebanon akiagiza kudumishwa mapambano ya aina mbalimbali dhidi ya utawala vamizi na wa Kizayuni wa Israel kwa wale wote wanaohisi kubeba dhima na wajibu huo mkubwa.
Habari ID: 3471242   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/11/01

TEHRAN (IQNA)-Mkuu wa masuala ya kigeni wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amesema kuwa, harakati hiyo ina hamu ya kustawisha uhusiano wake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyuga zote.
Habari ID: 3471229   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/10/24

TEHRAN (IQNA)- Tarehe 16Septemba ni kumbukumbu ya ukatili wa kinyama uliotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika kambi za Wapalestina za Sabra na Shatila mjini Beirut Lebanon.
Habari ID: 3471178   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/17

TEHRAN (IQNA)- Umoja wa Mataifa umeulaani utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuzuia maendeleo pamoja na kuzorotesha hali ya kibinadamu katika ardhi za Palestina zilizo katika eneo la Quds Mashariki, Ukingo wa Maghribi na Ukanda wa Ghaza katika kipindi cha zaidi ya miaka 50 ya kukalia kwa mabavu maeneo hayo.
Habari ID: 3471173   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/09/14

TEHRAN (IQNA)- Agosti 21 miaka 48 iliyopita, yaani mwaka 1969 Miladia, Msikiti wa al-Aqsa Kibla cha Kwanza cha Waislamu ulihujumiwa na kuteketezwa moto na Wazayuni kwa himaya ya utawala haramu wa Israel.
Habari ID: 3471136   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/08/22

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran
TEHRAN (IQNA)-Waziri wa Mambon ya Nje wa Iran amesema Jumuiya ya Ushirikiano wa nchi za Kiislamu OIC inapaswa kujikita katika malengo yake makuu ambayo ni kuimarisha umoja na mshikamano wa Kiislamu, kukomesha uvamizi wa Israel na kukaliwa kwa mabavu ardhi ya Palestina
Habari ID: 3471099   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/08/02

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Hija ni fursa bora ya mahali na wakati kwa Umma wa Kiislamu kutangaza misimamo kuhusu kadhia ya Palestina, msikiti wa Al-Aqsa na uwepo wenye malengo maovu wa Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.
Habari ID: 3471094   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/30

TEHRAN- (IQNA)-Askari wa utawala wa Kizayuni wa israel wamewavamia Wapalestina waliofanya mgomo wa kukaa kitako katika msikiti wa Al-Aqsa na kuwatia nguvuni zaidi ya watu mia moja.
Habari ID: 3471092   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/28

TEHRAN (IQNA)-Taasisi za Kiislamu Palestina zimechukua hatua za pamoja kupinga vizingiti vilivyowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Msikiti wa al-Aqsa.
Habari ID: 3471084   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/25

Jumuiya ya Nchi za Kiarabu
TEHRAN (IQNA)- Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imeutahadharisha utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba 'unacheza na moto' kutokana na kushadidisha ukandamizaji dhidi ya Wapalestina wa Quds Tukufu inayokaliwa kwa mabavu.
Habari ID: 3471082   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/24

TEHRAN (IQNA)-Wanajeshi 15,000 wa utawala wa Kizayuni wa Israel leo wameuzingira msikiti wa al-Aqsa na kuwazuia Waislamu kuswali Ijumaa huku kukiwa na sheria kali za usalama.
Habari ID: 3471077   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/21

TEHRAN (IQNA)-Ulimwengu wa Kiislamu umelaani hatua ya utawala haramu wa Israel ya kuufunga Msikiti wa al Aqsa katika mji wa Quds Tukufu (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu baada ya oparesheni ya Wapalestina dhidi wanajeshi wa Kizayuni karibu na msikiti huo.
Habari ID: 3471067   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/15

TEHRAN (IQNA)-Wapalestina watatu wamepigwa risasi na kuuawa katika oparesheni dhidi ya wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika mji unaokaliwa kwa mabavu wa Quds.
Habari ID: 3471066   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/14

Waziri Mkuu wa India safarini Tel Aviv
TEHRAN (IQNA)-Narendra Modi, Waziri Mkuu wa India anatembelea ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel na kukutana na wakuu wa utawala huo wa Kizayuni lakini hatakutana na viongozi wa Palestina.
Habari ID: 3471051   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/07/05

TEHRAN (IQNA)- Kumefanyika kikao cha siri mjini Cairo kati ya nchi kadhaa za Kiarabu na Utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu mustakabali wa eneo la Palestina la Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3471041   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/06/29

TEHRAN (IQNA) Waislamu na watetezi wa haki Tanzania na Kenya wameungana na wapigania haki duniani kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds ambayo ni Ijumaa ya mwisho ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3471033   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/06/24

TEHRAN (IQNA)-Jeshi la Utawala haramu wa Israel limeua shahidi watoto zaidi ya 3,000 Wapalestina tangu ulipoanza mwamako wa pili wa Wapalestina maarufu kama Intifadha mwezi Septemba 2000.
Habari ID: 3471004   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/06/02

TEHRAN (IQNA)- Jumuiya kubwa zaidi ya wafanyakazi Norway imetangaza kususia bidhaa za utawala wa Kizayuni wa Israel kulalamikia ukandamizaji unaofanya na utawala huo dhidi ya Wapalestina.
Habari ID: 3470978   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/05/13

TEHRAN (IQNA)-Kamati ya Utendaji ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Utamaduni na Sayansi UNESCO Jumanne ilipitisha azimio ambalo liliulaani utawala wa Kizayuni wa Israel kwa ajili ya kukiuka sheria za kimataifa katika mji wa Quds (Jerusalem) na Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3470966   Tarehe ya kuchapishwa : 2017/05/03