IQNA

Sayyid Hassan Nasrullah

Hizbullah ilivuruga mipango ya Wamagharibi

15:13 - May 26, 2014
Habari ID: 1411327
Sayyid Hassan Nasrullah Katibu Mkuu wa Harakati ya mapambano (Muqawama) ya Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon, amesema kuwa, Iddi au siku kuu ya muqawama na kukombolewa kusini mwa Lebanon ni Iddi ya taifa na umma mzima wa Kiislamu.

Sayyid Hassan Nasrullah aliyasema hayo Jumapili jioni katika hotuba aliyoitoa katika sherehe za kuadhimisha miaka 14 ya ushindi wa muqawama dhidi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na kuondoka utawala huo katika maeneo ya kusini mwa nchi hiyo ya Kiarabu. Alisisitiza kuwa, ushindi huo na mwingineo wa harakati ya muqawama dhidi ya Wazayuni, umepelekea kusambaratisha mpango wa Mashariki ya Kati mpya wa Marekani na utawala huo haramu.

Aidha amefafanua zaidi kuwa, ushindi huo ni ushindi wa Lebanon, Waarabu na umma mzima wa Kiislamu na kwamba hakuna kundi lolote linaloweza kujisifu kwamba ushindi huo ni wake pekee. Amesema, ni lazima kujiweka tayari kukabiliana na adui na kwamba muqawama hivi sasa ndio njia pekee ya kiulinzi kwa ajili ya tataifa hilo. Kwa upande mwingine Katibu Mkuu wa harakati ya muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon amesema kuwa, ili uweze kufikia mafanikio yake katika kuwalinda wananchi, taifa na serikali ya Lebanon, muqawa unahitajia msaada wa kirafiki wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Syria hasa kwa kuzingatia kuwa, adui Mzayuni amejizatiti vilivyo.

1410885

captcha