Akizungumza Jumamosi, amesema kauli ya Macron inaweza kuibua migongan baina ya wafuasi wa dini mbali mbali duniani katika kipindi hiki ambacho dunia inahitaji umoja ili kukabiliana na janga la COVID-19.
“Uhuru wa maoni haupaswi kutumiwa kwa njia ambayo inavunjia heshima matukufu ya kidini,” aliongeza rais wa Indonesia katika mkutano na waandishi habari kwa njia ya intaneti.
Aidha alilaani vikali hujuma za kigaidi ambazo zilijiri Paris na Niece Ufaransa na kusema Indonesia inatoa wito wa umoja na kustahamiliana kidini kwa ajili ya kujenga dunia bora.
Rais wa Indonesia amebainisha masikitiko yake kuwa Macron amenasibisha hujuma za kigaidi na Uislamu na kusema hilo ni kosa kubwa. “Ugaidi ni ugaidi. Magaidi ni magaidi. Ugaidi hauna uhusiano wowote na dini yoyote ile,” ameongeza.
Rais Macron wa Ufaransa anaendelea kukosolewa na Waislamu kimataifa kutokana na matamshi yake ya kuutusi Uislamu na Mtume Muhammad SAW. Matamshi hayo yameibua maandamano ya kumlaani huku kukianzishwa kampeni ya kutaka bidhaa zote za Ufaransa zisusiwe.