TEHRAN (IQNA) - Wimbi kali la maandamano ya kulaani matamshi yaliyotolewa na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akitetea matusi na kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad SAW Nchini humo limeendelea kushuhudiwa katika pembe mbalimbali za dunia.
Wanaoshiriki katika maandamano hayo aidha wametaka bidhaa za Ufaransa zisusiwe kama njia ya kuwaadhibu watawala wa nchi hiyo wenye chuki dhidi ya Uislam na Waislamu.