Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa imesema shambulio hilo lilitokea katika makaburi ya wasiokuwa Waislamu katika mji Jeddah ulioko katika Bahari ya Sham.Hata hivyo, wizara hiyo haikutoa maelezo zaidi juu ya idadi ya majeruhi au uraia wako.
Kufuatia hujuma hiyo, Ubalozi wa Ufaransa katika Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE, umewataka raia wake kuwa macho baada ya kutokea shambulio katika mji wa Jeddah. Taarifa kutoka ubalozi huo imesema, Ufaransa inawasiliana na mamlaka za UAE ili kuhakikisha raia wake wako salama.
Hujuma hiyo ya Jumatano inakuja huku Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akiendelea kuwakasirisha Waislamu duaniani baada ya kuunga mkono wale wanaomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW katika nchi hiyo ya Ulaya.
Waislamu duniani wameandamana kote duniani kumlaani mtawala huyo wa Ufaransa huku wakitaka bidhaa za Ufaransa zisusiwe.