Akademia hiyo imefunguliwa na Sheikh Sultan bin Muhammad al Qasimi ambaye ni kiongozi mkuu wa Sharjah.
Akademia hiyo imejengwa katika eneo lenye ukubwa wa mita mraba 75,000 na ina majumba ya makumbusho saba ya kihistoria na kisayansi.
Akizungumza katika ufunguzi huo, kiongozi mkuu wa Sharjah amesema Akademia ya Qur’ani Tukufu Sharjah ni eneo lenye harakati nyingi zenye kutoa maarifa kuhusu Qur’ani Tukufu.