IQNA

Wiki ya Umoja wa Kiislamu

Rais wa Iran asisitiza kuhusu umoja wa Kiislamu ili kukabiliana na jinai za Israel

19:07 - September 19, 2024
Habari ID: 3479453
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, adui analeta mgawanyiko na mifarakano kati yetu na kubainisha kwamba, Waisraeli milioni 2 au 3 wanawaangamiza Waislamu, wanaua wanawake na watoto, wazee na vijana na wagonjwa, wanapiga mabomu hospitali na misikiti na sisi tumekaa tu na kutazama, kwa sababu hatuna umoja na ndio maana Israel inathubutu kufanya jinai hizi.

Rais Masoud Pezeshkian amesema hayo hapa mjini Tehran katika Kongamano la 38 la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu lililohudhuriwa na wanafikra na wanazuoni kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu, na kusisitiza kwamba, ni lazima tushikane mkono, umoja na mshikamano wa sisi Waislamu unaongeza nguvu zetu.

Rais Pezeshkian ameongeza kuwa, Israel inatenda jinai kwa sababu hatuna maono na lugha moja sisi kwa sisi, hatuna umoja wa Kiislamu, tunapigania mambo mepesi, Sala na saumu ni kwa ajili ya umoja, kama hamna umoja baina yenu mnafunga na kuswali kwa ajili ya nini?

Mkutano wa 38 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu unaofanyika chini ya kaulimbiu  "Ushirikiano wa Kiislamu ili Kufikia Thamani za Pamoja kwa Kutilia Mkazo Suala la Palestina" umeanza hapa Tehran kwa kuhudhuriwa na wageni 2,500 mbalimbali wakiwemo shakhsia wa kijeshi na pia wasomi na wanafikra wa nchi za Kiislamu.

Siku ya 17 ya Rabiul Awwal, ambayo ni Septemba 21 mwaka huu, inaaminika na Waislamu wa madhehebu ya Shia kuwa siku ya kukumbuka kuzaliwa kwa Mtume Mohammad (SAW), wakati Waislamu wa Sunni wanaamini tarehe sahihi ni 12 Rabiul Awwal

Muda kati ya tarehe hizo mbili huadhimishwa kila mwaka kama Wiki ya Umoja wa Kiislamu.

Hayati Mwanzilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Imam Khomeini (RA) ndiye alitangaza muda baina ya tarehe hizo mbili kuwa Wiki ya Umoja wa Kiislamu nyuma katika miaka ya 1980.

3489962

Habari zinazohusiana
captcha