Miongozo hiyo ilichapishwa kama infografiki kwenye akaunti rasmi ya Mamlaka hiyo kwenye X, jukwaa lililojulikana hapo awali kama Twitter.
Wageni wa kike wanahimizwa kuzingatia taratibu maalum wakati wakiwa kwenye maeneo ya Swala. Ushauri huo unasisitiza umuhimu wa kuvaa mavazi yanayofaa ya Kiislamu, kushirikiana na wafanyakazi wa msikiti, na kuepuka shughuli kama kulala au kupumzika katika maeneo ya Swala.
Pia inasisitiza kudumisha mistari iliyonyooka katika safu za Swala. Maelekezo mengine ni pamoja na kudumisha usafi, kuepuka kula au kunywa ndani ya maeneo ya Swala, kupunguza viwango vya kelele, na kuhakikisha viatu havivaliwi kwenye mazulia.
Aidha, Mahujaji wanashauriwa kuweka mali zao binafsi salama na kuepuka kuziacha bila uangalizi.
Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, miongozo hiyo inalenga kuhifadhi utakatifu wa maeneo hayo matakatifu huku ikiboresha hali ya waumini wote.
Hatua hizo zinaonyesha juhudi pana za kuhudumia mamilioni ya Mahujaji wanaotembelea misikiti mitakatifu kila mwaka, hasa wakati wa vipindi vya kilele kama vile Ramadhani na Hija.
3490956