IQNA

Kamanda wa IRGC: Kutekeleza Qur'ani Tukufu Kunazuia Kushindwa

9:37 - March 12, 2025
Habari ID: 3480356
IQNA – Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema Waislamu hawatashindwabikiwa watafuata mafundisho ya Qur'ani Tukufu.

"Mradi tunatenda kulingana na mafundisho na amri za Quran, hatutashindwa," alisema Meja Jenerali Hossein Salami, akihutubia tamasha la Qur'ani Tukufu la IRGC huko Tehran Jumatatu.
Alirejelea ushindi wa watu wa Ukanda wa Gaza kama mfano, akisema walipambana na utawala wa Kizayuni kwa miezi 16 wakikabiliana na mabomu, mzingiro, baridi na magumu, na hatimaye walishinda.
Watu wa Yemen ambao wamesimama dhidi ya adui mwenye kiburi bila hofu ni mfano mwingine, amesema kamanda wa IRGC.
Meja Jenerali Salami pia alisema IRGC ni taasisi ya Qur'ani ambayo imeundwa na mizizi ya kina ya imani, na matawi yake yameenea kote ulimwenguni, yakitangaza uhuru, heshima, na usalama kwa Waislamu waliodhulumiwa.

732105

 

Kishikizo: qurani tukufu irgc
captcha