marekani - Ukurasa 5

IQNA

IQNA-Jamii ya wakazi na majirani wa jiji la Norfolk, jimbo la Virginia nchini Marekani, wamejitokeza kwa wingi kusafisha na kurejesha hadhi ya Msikiti wa Masjid Ash Shura baada ya kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki, huku polisi wakiomba msaada wa umma kumtambua mtuhumiwa.
Habari ID: 3481650   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/12

IQNA – Jukwaa la kimataifa litakalojadili mkutano wa hivi karibuni wa tafiti za Qur’ani uliofanyika Los Angeles litafanyika mtandaoni leo na Jumamosi ijayo kupitia jukwaa la Zoom.
Habari ID: 3481626   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/07

IQNA – Jeshi la Polisi wa Kaunti ya Richland limethibitisha kukamatwa kwa mwanamume aliyeingia msikiti mmoja wa South Carolina, Marekani, wakati wa sala huku akiwa na bunduki aina ya AR-15.
Habari ID: 3481552   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/22

IQNA – Wanafunzi Waislamu katika Chuo Kikuu cha Florida Kusini (USF) nchini Marekani wamesema wanaume watatu walivuruga mkusanyiko wao wa sala ya alfajiri na kuwatendea unyanyasaji.
Habari ID: 3481550   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/21

IQNA – Waandamanaji waligongana mitaani Dearborn Jumanne baada ya wanaharakati wa mrengo wa kulia kuwachokoza wakazi kwa kauli za chuki dhidi ya Uislamu na wahamiaji, na kujaribu kudhalilisha Qur'ani Tukufu. Tukio hilo lilisababisha msuguano mdogo na polisi kuingilia kati kwa nguvu ili kuwatenganisha makundi hayo.
Habari ID: 3481539   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/19

IQNA – Baada ya tukio la uhalifu wa chuki lililoripotiwa ambapo dada Muislamu alivamiwa na kufuatwa karibu na Chuo Kikuu cha Columbia kwa sababu ya kuvaa niqab, taasisi hiyo imetoa tamko la kulaani shambulio hilo hadharani.
Habari ID: 3481522   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/16

IQNA – Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amejibu ripoti ya gazeti la New York Times kuhusu kufukuzwa kwa baadhi ya majenerali wa Marekani kwa kunukuu aya ya Qur’ani Tukufu.
Habari ID: 3481502   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/11

IQNA – Chuo Kikuu cha Houston kilichopo jimbo la Texas, Marekani, kimetangaza kuwa kinachunguza tukio la kuvunjia heshima nakala ya Qur'an Tukufu wakati wa mkusanyiko wa wanafunzi Waislamu.
Habari ID: 3481472   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/05

IQNA-Maandamano ya Siku ya Mwenyezi Mwenyezi Mungu yaani Aban 13 ambayo ni Siku ya Taifa ya Iran ya Kupambana na ubeberu na uistikbari yamefanyika hapa mjini Tehran na katika zaidi ya miji 900 kote humu nchini.
Habari ID: 3481465   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/04

IQNA-Mwandishi wa habari raia wa Uingereza anayejulikana kwa kuunga mkono Palestina amekamatwa nchini Marekani na shirika la Uhamiaji na Forodha (ICE), kufuatia shinikizo kutoka kwa makundi yanayoiunga mkono Israel.
Habari ID: 3481430   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/28

IQNA – Watawala wa Marekani wanaficha na kuziba hofu yao dhidi ya vuguvugu la wananchi nchini humo, amesema Mkuu wa Taasisi ya Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu (ICRO).
Habari ID: 3481422   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/27

IQNA – Jumuiya ya Waislamu wa jiji la Winnipeg, mji mkuu wa jimbo la Manitoba nchini Kanada (Canada), walikusanyika mwishoni mwa wiki hii kusherehekea ufunguzi rasmi wa msikiti mpya katika jiji hilo.
Habari ID: 3481392   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/21

IQNA-Katika mji wa Mason, jimbo la Ohio nchini Marekani, kuna shule inayojulikana kama ICM Learning Academy ambayo hufundisha wanafunzi si tu kusoma Qur’ani Tukufu bali pia kuifahamu na kuikumbuka kwa moyo wote.
Habari ID: 3481384   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/19

IQNA – Viongozi wa jamii ya Kiislamu mjini Minneapolis wanatoa wito wa uchunguzi wa kina kuhusu iwapo tukio la uvunjaji wa hivi karibuni katika Kituo cha Kiislamu cha Alhikmah linahusiana na tukio la moto lililotokea siku chache kabla katika msikiti huo huo.
Habari ID: 3481343   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/08

IQNA – Tukio la moto katika Msikiti wa Kituo cha Kiislamu Alhikma, ulioko Mtaa wa 32 kusini mwa Minneapolis, limezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa viongozi wa Kiislamu, ambao sasa wanatoa wito wa uchunguzi wa kina, licha ya mamlaka za zimamoto kusema kuwa tukio hilo lilikuwa la bahati mbaya.
Habari ID: 3481310   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/01

IQNA-Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani mashambulizi ya anga ya “kikatili” yaliyofanywa na Marekani na Israel mwezi Juni katika ardhi ya Iran na kusema yalikuwa usaliti kwa diplomasia.
Habari ID: 3481282   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/25

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amepinga ombi la Washington la mazungumzo ya nyuklia na kusema kwamba hakuna taifa lolote huru na lenye heshima linaloweza kukubali mazungumzo chini ya mashinikizo.
Habari ID: 3481281   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/24

IQNA – Wakazi wa Plainfield, jimbo la Illinois, walikusanyika Jumapili kuadhimisha siku maalum ya kumkumbuka Wadee Alfayoumi, mtoto wa miaka sita mwenye asili ya Kipalestina na Mmarekani aliyeuawa katika tukio la chuki takriban miaka miwili iliyopita.
Habari ID: 3481266   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/22

IQNA – Mjumbe wa chama cha Democratic katika Bunge la Marekani, Bi Ilhan Omar, amesisitiza utambulisho wake wa Kiislamu, akisema anajivunia kuwa Mwislamu.
Habari ID: 3481264   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/21

IQNA – Polisi wa McKinney, Texas, walifika wiki hii katika eneo la tukio la uhalifu lililotokea katika kituo cha elimu ya Kiislamu ambacho kikundi cha kutetea Waislamu kimekitaja kuwa ni unyanyasaji wa chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3481259   Tarehe ya kuchapishwa : 2025/09/20