iqna

IQNA

Watetezi wa Palestina
IQNA - Mamia ya watu walikusanyika katika Kituo cha Kiislamu cha Maine siku ya Jumapili kuwaandikia barua wawakilishi wao, wakiwataka kuunga mkono takwa la kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel usitisha vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Gaza. Wapalestina wasiopungua 26,000 wameuawa shahidi tangua utawala wa Israel uanzishe vita dhidi ya Gaza Oktoba mwaka jana.
Habari ID: 3478273    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/29

Jinai za Israel
IQNA-Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ hii leo imeamua kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel lazima uchukue hatua zote za kuzuia vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi yake dhidi ya Wapalestina huko, Gaza.
Habari ID: 3478258    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/26

Al Houthi
IQNA-Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen Abdul-Malik al-Houthi anasema kulengwa kwa meli zinazohusishwa na utawala wa Kizayuni wa Israel kutaendelea katika Bahari ya Sham hadi Wapalestina walioko Gaza watakapoweza kupokea misaada.
Habari ID: 3478254    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/26

Harakati za Qur'ani
IQNA - Kijana wa Kipalestina amezindua mpango wa kusambaza nakala za Qur’ani Tukufu miongoni mwa wale wanaoishi katika kambi za wakimbizi katika eneo la Gaza ambalo linakabiliwa na mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3478253    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/25

Kadhia ya Palestina
IQNA-Afrika Kusini imesema inatazamia hukumu ya awali ya kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza itatolewa Ijumaa.
Habari ID: 3478251    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/25

Jinai za Israel
IQNA-Ripota wa Umoja wa Mataifa anasema utawala wa Kizyuni wa Israel unatumia njaa kama silaha dhidi ya watu Wapalestina wa Gaza ambao wanakabiliwa na mgogoro mkubwa wa chakula baada ya miaka ya vikwazo na vita vya sasa vya maangamizi ya umati vinavyotekelezwa na Israel.
Habari ID: 3478241    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/23

Jinai za Israel
IQNA - Wapiga kura wa Marekani wamehimizwa kuandika "Sitisha Vita Gaza" kwenye kura zao wakati wa kuchagua wagombea wa uchaguzi wa rais wa mwezi Novemba ikiwa ni njia ya kubainisha malalamiko kuhusu jinsi Joe Biden alivyoshughulikia vita vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Gaza.
Habari ID: 3478238    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/23

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza katika kikao cha maimamu wa Ijumaa kote Iran kuwa: Watu madhulumu na wenye nguvu wa Ghaza wameweza kuwaathiri walimwengu kwa mapambano yao.
Habari ID: 3478205    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/16

Kiongozi wa Hizbullah
IQNA-Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon Hizbullah amesema utawala haramu wa Israel mepata hasara "isiyo na kifani" mikononi mwa makundi ya Kiiislamu ya kupigania ukombozi wa Palestina (muqawama) na imeshindwa kufikia malengo yake yoyote baada ya siku 100 za vita vyake vya mauaji ya kimbari kwenye Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478199    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/15

Watetezi wa Palestina
IQNA- Nchi zaidi zimeungana na Afrika Kusini katika kesi iliyowasilishwa dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu vita vya mauaji ya kimbari vya utawala huo kwenye dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.
Habari ID: 3478182    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/11

Jinai za Israel
IQNA-Spika wa Bunge la Iran Mohammad Baqer Qalibaf anasema utawala wa Kizyauni wa Israel uliasisiwa kwa mauaji ya kimbari na vita na hivyo kuendelea kuwepo kwake kunategemea kutekeleza jinai hizo za kutisha.
Habari ID: 3478179    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/10

Watetezi wa Palestina
IQNA - Mashirika kadhaa ya Kiislamu nchini Kanada (Canada) yamemuomba Waziri Mkuu Justin Trudeau kuunga mkono uchunguzi wa kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita wa utawala wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3478177    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/10

Jitihada
IQNA - Licha ya mashambulizi ya mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza ambayo yamepelekea watu ya 23,000 kupoteza maisha na malaki kuyahama makazi yao, mafunzo ya Qur'ani Tukufu yanaendelea katika eneo hilo lililozingirwa.
Habari ID: 3478163    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/07

Watetezi wa Palestina
IQNA – Makumi ya makundi na mashirika ya kijamii nchini Marekani yametangaza azma ya kushiriki katika maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika Washington, DC, kuunga mkono Wapalestina wanaodhulumiwa na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3478158    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/06

Jinai za Israel
IQNA – Jinamizi ambalo watoto wa Gaza wanapitia linazidi kuwa mbaya siku hadi siku, mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) alisema.
Habari ID: 3478156    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/06

Jinai za Israel
IQNA - Idara ya Wakfu ya Kiislamu, inayosimamia Msikiti wa Al-Aqsa huko al-Quds (Jerusalem), imesema leo kwamba ni waumini 15,000 pekee walioruhusiwa kuingia katika eneo hilo takatifu kwa ajili ya Sala ya Ijumaa kutokana na vikwazo vilivyowekwa na utawala ghasibu wa Israel.
Habari ID: 3478154    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/05

Jinai za Israel
IQNA-Mashtaka ya Afrika Kusini dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) kuhusu tuhuma za mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza kuanza kusikilizwa wiki ijayo.
Habari ID: 3478147    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/04

Jinai ya Israel
IQNA-Naibu mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Palestina Hamas ameuawa katika shambulio la kigaidi la ndege isiyo na rubani ya utawala katili wa Israel katika kitongoji cha kusini mwa mji mkuu wa Lebanon wa Beirut.
Habari ID: 3478137    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/03

IQNA - Wanazuoni waandamizi wa Kiislamu nchini Yemen katika taarifa wamesisitiza kuwa ni Haramu kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3478131    Tarehe ya kuchapishwa : 2024/01/02

Jinai za Israel
IQNA - Zaidi ya maeneo 200 ya kiakiolojia na ya kale katika Ukanda wa Gaza yameharibiwa na uvamizi wa kijeshi wa Israel tangu Oktoba 7, kulingana na mamlaka huko Gaza.
Habari ID: 3478117    Tarehe ya kuchapishwa : 2023/12/31