IQNA - Waziri wa Ulinzi wa India Rajnath Singh alihimizwa na kundi la watu mashuhuri kusitisha mara moja usafirishaji wa silaha kwenda Israel, ambayo inaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki kwenye Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3479228 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/08/04
Jinai za Israel
IQNA-Wito unaongezeka kote ulimwenguni wa kuipiga marufuku timu ya utawala haramu wa Israel kushiriki Michezo ya Olimpiki ya Paris 2024 inayoanza Ijumaa huku utawala huo ukiendeleza vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya raia Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3479182 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/25
Kadhia ya Yemen
Yemen ina uwezo mkubwa zaidi wa kukabiliana na mapigo kwa utawala wa Israel, amesema kiongozi wa Ansarullah wa Yemen huku operesheni za kulipiza kisasi za nchi hiyo ya Kiarabu zikiendelea kuwaunga mkono Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3479168 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/22
Utawala wa Kizayuni
Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon ametoa aya za Qur'ani Tukufu na kusisitiza kwamba mwisho wa utawala mbovu wa Israel utakuja mapema zaidi kuliko baadaye.
Habari ID: 3479139 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/17
Kadhia ya Palestina
Anwar El Ghazi ameshinda kesi dhidi ya klabu ya Ujerumani ya Bundesliga Mainz 05, ambayo ilikatisha kandarasi yake kwa kuunga mkono Palestina, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya Ujerumani.
Habari ID: 3479119 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/14
Kadhia ya Palestina
Wanaharakati wa kitamaduni na wasanii wa nchi za Magharibi wamekabiliwa na matatizo baada ya kueleza mshikamano wao na Gaza na kuchukua misimamo dhidi ya vita vya mauaji ya kimbari ya Israel.
Habari ID: 3479065 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/04
Kadhia ya Palestina
Mteule katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Marekani alijiuzulu siku ya Jumanne, akitolea mfano "ushirikiano" wa utawala wa Joe Biden katika mauaji ya kimbari ya Gaza ambapo takriban watu 37,900 wameuawa tangu Oktoba 7,2023 mwaka jana.
Habari ID: 3479059 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/03
Kadhia ya Palestina
Mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa ya Gaza, Dk. Muhammad Abu Salmiya, aliachiliwa kutoka kizuizini cha Israeli siku ya Jumatatu baada ya kipindi cha miezi saba.
Habari ID: 3479045 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/07/01
Mauaji ya Kimbari huko Gaza
Waandamanaji huko Washington, DC, wamelaani mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3479015 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/26
kadhia ya Palestina
Afisa wa Hamas alisema pendekezo lolote la kusitisha mapigano ambalo halijumuishi kumalizika kwa vita vya Israel dhidi ya Gaza litakataliwa na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas.
Habari ID: 3479007 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/24
Kadhia ya Palestina
IQNA-Marekani na utawala wa Kizayuni zinatekeleza sera ya njaa katika Ukanda wa Gaza ili kuhakikisha Wapalestina wa eneo hilo wanaagamia kutokana na ukosefu wa chakul, maafisa katika eneo hilo la Palestina walisema.
Habari ID: 3478990 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/20
Utawala katili wa Israel
Mwanazuoni wa Kiisalmi ,iraq alilitaja wazo la kuhalalisha au kuanzisha uhusiano w kawaida kati ya nchi hiyo ya Kiarabu na utawala wa Kizayuni kuwa jambo lisilowezekana.
Habari ID: 3478985 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/19
IQNA -Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imepokea vizuri kupitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa azimio ambalo limeunga mkono mpango unaolenga kuleta usitishaji mapigano katika vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3478961 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/11
Jinai za Israel
IQNA-Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ametahadharisha kuwa, Israel inapasa kusubiri jibu la Iran kwa kumuua shahidi mmoja wa washauri wa kijeshi wa Jamhuri ya Kiislamu katika uvamizi wa utawala huo wa Kizayuni katika mji wa Aleppo (Halab) huko kaskazini magharibi mwa Syria.
Habari ID: 3478941 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/07
Jinai za Israel
IQNA - Mufti katika jumuiya ya Kiislamu ya Serbia anasema kukabiliana na jinai zinazoendelea za Israel huko Gaza ni jukumu la wanadamu wote.
Habari ID: 3478934 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/05
Jinai za Israel
IQNA – Utawala ghasibu wa Israel umegeuza mji unaokaliwa kwa mabavu wa al-Quds (Jerusalem) kuwa eneo la kijeshi kwa kisingizio cha kufanikisha mjumuiko wa kichochezi unajulikana kama "maandamano ya bendera". Mjumuiko huu umepengwa jumuiya za kikoloni siku ya Jumatano.
Habari ID: 3478929 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/04
IQNA - Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imetoa onyo kali kwamba misaada ya kutosha ya kibinadamu haiwafikii Wapalestina huko Gaza, na kusababisha visa vikali vya njaa miongoni mwa watoto.
Habari ID: 3478924 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/04
Muqawama
IQNA-Kiongozi wa harakati ya muqawama ya Hizbullah ya Lebanon ametaka juhudi za kimataifa za kuutokomeza utawala wa Kizayuni, akisema ni utawala huo ni 'uvimbe wa saratani" ambao lazima uondolewe.
Habari ID: 3478910 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/06/01
Muqawama
IQNA-Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuhusu mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel huko Rafah kusini mwa Ukanda wa Ghaza kwamba, jinai hiyo ya kutisha uliyofanya utawala huo ghasibu inapasa iwaamshe na kuwatoa kwenye usingizi wa mghafala watu waliojisahau duniani na walioshindwa kuwa na msimamo.
Habari ID: 3478901 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/05/29
Jinai za Israel
IQNA-Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) imeutaka Utawala wa Kizayuni wa Israel usitishe mashambulizi yake katika mji wa kusini wa Gaza wa Rafah na kujiondoa katika eneo hilo, katika kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini ikiishutumu Israel kwa kufanya mauaji ya kimbari, na kuielezea hali hiyo kuwa ni hatari kubwa kwa wakazi wa Palestina.
Habari ID: 3478881 Tarehe ya kuchapishwa : 2024/05/25