Mashabiki wa Ufaransa wameripotiwa kuendesha mashambulizi ya kibaguzi dhidi ya Mohamed Youcef Belaïli, winga wa Brest, katika mechi dhidi ya Reims siku ya Jumapili.
Ikilaani mashambulizi hayo, shirikisho hilo lilionyesha uungaji mkono wake kamili kwa Belaïli.
Tabia hii ya kishenzi ni tofauti na roho ya mchezo wa haki, lilibaini shirikisho hilo.
Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya 1-1 na mashambulizi ya maneno yaliiibuka baada ya Belaïli kukosa penalti katika dakika ya 53. "Hii ni Ufaransa, rudi nchini kwako" iliripotiwa kuwa moja ya nyimbo za kibaguzi.
Katika taarifa baada ya mechi hiyo, Brest alitangaza kwamba uchunguzi wa madai hayo utafunguliwa kwa ushirikiano wa Reims.
Chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu zimeongezeka katika miaka ya hivi karibuni huku serikali ikionekana kufuata sera rasmi za kuwagbagua Waislamu.