IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Mashindano ya Qur’ani ya wanachuo wa Iran yaanza Tabriz

20:36 - September 10, 2024
Habari ID: 3479412
IQNA - Toleo la 38 la Mashindano ya Qur'an na Etrat kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vya Iran lilizinduliwa katika mji wa kaskazini magharibi wa Tabriz siku ya Jumatatu.

Chuo Kikuu cha Tabriz cha Sayansi ya Tiba kinaandaa hafla ya mwaka huu ya Kurani.

Jumla ya washindani 277 wanawania tuzo ya juu katika kategoria tofauti katika sehemu za wanaume na wanawake.

Hao ndio wametinga fainali baada ya kuonesha kiwango bora katika hatua za awali.

Tarteel, usomaji wa Qur’ani, kuhifadhi Qur'ani katika viwango tofauti, usomaji wa mashairi ya kidini na dua ni kati ya kategoria za mashindano hayo.

3489831

Jumla ya wataalamu 45 wa Qur’ani wanahudumu katika majopo ya majaji katika sehemu za wanaume na wanawake.

Mashindano hayo yataendelea hadi Jumatano, Septemba 11, 2024.

Hafla hiyo ya kila mwaka huandaliwa kwa pamoja na Wizara ya Sayansi, Utafiti na Teknolojia na Wizara ya Afya na Sayansi ya Tiba.

Inalenga kukuza mafundisho ya Qur'ani miongoni mwa wanafunzi wa vyuo vikuu.

Habari zinazohusiana
captcha