IQNA

Qari Muirani asoma Qur’ani katika Tuzo ya Kimataifa ya Al-Ameed Nchini Iraq

20:52 - March 05, 2025
Habari ID: 3480311
IQNA – Qari Rahim Sharifi kutoka Iran alisoma Qur’ani katika toleo la pili la Shindano la Kimataifa la Kisomo cha Qur’an la Al-Ameed, ambalo linaendelea katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq. Sharifi anatoka mji wa Ramhormoz katika mkoa wa kusini-magharibi wa Khuzestan.

Alizaliwa mwaka wa 1985, alijifunza usomaji wa Qur’an kutoka kwa kaka yake Reza Sharifi. Rahim ameshinda mara kadhaa katika mashindano ya Qur’ani ya Iran. Pia ni mwanachama wa kikundi cha Sabtayn Tawasheeh na ameshinda zawadi katika mashindano mbalimbali ya Tawasheeh. Raundi ya mwisho ya toleo la pili la Shindano la Kimataifa la Kisomo cha Qur’an la Al-Ameed ilizinduliwa Karbala na kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Qari kutoka nchi 22 wanashiriki katika tukio hilo la kimataifa la Qur’ani. Katika raundi ya kwanza, watu waliovutiwa waliwasilisha kipande cha video cha kisomo chao kwa kamati ya shindano na wale waliokuwa na utendaji bora walifika fainali.

Toleo la kwanza la Shindano la Kimataifa la Kisomo cha Qur’an la Al-Ameed katika Ramadhani yam waka jana lilivutia washiriki kutoka nchi 21. Linaandaliwa na Idara ya Mfawidhi wa Kaburi la Hadhrat Abbas (AS) kwa lengo la kukuza utamaduni wa Qur’ani.

3492166

Habari zinazohusiana
captcha