IQNA

Bendera za Maombolezo ya Ashura Zikiwa zimepandishwa kwenye Haram Takatifu huko Karbala

19:56 - July 09, 2024
Habari ID: 3479098
IQNA - Bendera nyekundu za Haram (kaburi) Tukufu ya mam Hussein (AS) na Aba Al- Fadhl Al-Abbas (AS) zilishushwa na bendera nyeusi za maombolezo zikapandishwa kwenye majumba ya makaburi hayo siku ya Jumatatu huko Iraq Karbala.

Leo ni siku ya kwanza ya mwezi wa Hijri wa Muharram nchini Iraq. 

Mustafa Murtadha Ziyaeddin, mfawidhi wa kaburi la Aba Al- Fadhl Al-Abbas (AS) huko Karbala, alibadilisha bendera nyekundu katika kaburi hilo na ile nyeusi  kulingana na mila ya muda mrefu.

Bendera nyeusi inaashiria maombolezo ya Waislamu wa Shia kwa ajili ya kuuawa shahidi Imam wa tatu (AS).

Muharram ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya mwandamo ya Hijri.

Waislamu wa madhehebu ya Shia na wengineo katika sehemu mbali mbali za dunia huomboleza kila mwaka katika mwezi wa Muharram katika kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Hussein (AS) na masahaba zake.


Bendera ya Haram ya Imam Ridha (AS) nchini Iran nayo pia Ilibadilishwa katikati ya Maandalizi ya Muharram
Imamu wa tatu wa Shia ambaye ni  Imamu Hussein (AS) na kikundi kidogo cha wafuasi wake na wanafamilia wake waliuawa kishahidi na kidhalimu katika zama utawala wa Yazid Bin Muawiya, katika vita vya Karbala katika siku ya kumi ya Muharram (ijulikanayo kama Ashura) mwaka wa 61 Hijria sawa 680 Miladia.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

3489049

 

 

 

Kishikizo: karbala ashura
captcha