IQNA

Nchi 22 zinashiriki Tuzo ya Pili ya Kimataifa ya Usomaji wa Qur’ani ya Al-Ameed

15:36 - March 03, 2025
Habari ID: 3480295
IQNA – Raundi ya mwisho ya toleo la pili la Mashindano ya Kimataifa ya Usomaji wa Qurani ya Al-Ameed ilizinduliwa katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq na kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Maqari kutoka nchi 22 wanashiriki katika tukio hilo la kimataifa la Qur’ani, Al-Kafeel iliripoti.

Kulingana na Ala al-Mousawi, naibu mkuu wa Baraza  la Kitaalamu la Qur’ani la Idara ya Mfawidhi wa Kaburi la Hadhrat Abbas (AS) nchini Iraq, kuna maqari kumi wanaoshindana katika sehemu ya vijana na 30 katika sehemu ya watu wazima.

Iran, Indonesia, Afghanistan, Malaysia, Afrika Kusini, India, na Misri ni miongoni mwa nchi zinazoshiriki.

Al-Mousawi alisema Kamati ya Mashindano ya Kimataifa inasimamia shindano hilo kulingana na viwango vya kimataifa.

Katika raundi ya kwanza, watu walionyesha shauku ambapo walitoa klipu ya video ya usomaji wao kwa kamati ya mashindano na wale waliofanya vizuri zaidi walifika fainali.

Toleo la kwanza la Mashindano ya Kimataifa ya Usomaji wa Qurani ya Al-Ameed katika Ramadhani 2024 lilivutia washiriki kutoka nchi 21.

Yanaandaliwa na Idara ya Mfawidhi wa Kaburi la Hadhrat Abbas (AS) kwa lengo la kukuza utamaduni wa Qur’ani.

3492136

Habari zinazohusiana
captcha