Mashindano hayo yaliandaliwa na Idara ya Masuala ya Kidini ya Ofisi ya Uongozi wa Msikiti Mkuu wa Bosnia na Herzegovina.
Ujumbe wa wajumbe na wawakilishi wa Mashindano ya Qur’ani ya Sheikh Jassim bin Mohammed bin Thani, yaliyo chini ya Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Qatar, ulishiriki katika ufunguzi wa hafla hiyo.
Sherehe ya ufunguzi ilihudhuriwa na idadi kubwa ya viongozi na watu wa dini kutoka ndani na nje ya Bosnia na Herzegovina, na ikasisitizwa kuwa ushiriki wa Qatar unaonesha kuendelea kwa msaada wake kwa mashindano ya Qur’ani nchini Bosnia na Herzegovina kwa mwaka wa tatu mfululizo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Husein Kavazovic, Mkuu wa Ulema wa Msikiti Mkuu wa Kiislamu wa Bosnia, alisisitiza kuwa msaada wa Qatar kwa mashindano haya unaakisi kina cha uhusiano wa kindugu kati ya nchi hizo mbili na una nafasi muhimu katika kuasisi dhana za Qur’ani na kueneza utamaduni wa Qur’ani miongoni mwa vizazi.
Aliongeza kuwa Qur’ani Tukufu si kitabu cha kusomwa tu, bali ni namna ya maisha na chanzo cha kudumu cha uongofu, elimu na maadili mema.
Akitaja kuwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu hubeba ujumbe wa milele wa imani na hekima ya kina, na kinachukuliwa kuwa rejea ya maendeleo ya mtu binafsi na jamii, Kavazovic alisema kuhifadhi Qur’ani na kusambaza mafundisho yake ni miongoni mwa majukumu ya juu kabisa ya wanaharakati wa Qur’ani.
Alifafanua kuwa mashindano haya yanalenga kuimarisha nafasi ya kuhifadhi na kusoma Qur’ani Tukufu nchini Bosnia na Herzegovina, na kuwahamasisha vijana kushindana katika kuhifadhi Kitabu cha Mwenyezi Mungu, kubadilishana uzoefu, na kujiandaa kushiriki katika mashindano ya kimataifa ya Qur’ani, jambo litakalosaidia kuibua kizazi cha Qur’ani chenye uwezo wa kuifikisha Uislamu kwa ufasaha.
Sheikh Abdulrahman bin Abdulaziz Al Thani pia alisema kuwa Serikali ya Qatar imefanya utumishi kwa Qur’ani Tukufu kuwa miongoni mwa majukumu yake muhimu zaidi, na imejikita kusaidia miradi inayodumisha maadili ya Kiislamu na kuchangia katika ujenzi wa ubinadamu kwa msingi wa mafundisho ya Qur’ani.
Alisisitiza kuwa mashindano haya yamepiga hatua kubwa mwaka hadi mwaka, jambo linaloonesha kuimarika kwa malengo yake ya juu; jitihada za kuimarisha uhusiano wa jamii ya Kiislamu na Kitabu cha Mwenyezi Mungu; kuhimiza kuhifadhi, kutafakari na kufuata Qur’ani; na kusaidia kuandaa kizazi bora cha Qur’ani kinachoakisi Qur’ani katika elimu, matendo na maadili.
3498346