waislamu - Ukurasa 99

IQNA

Taasisi ya juu zaidi ya Waislamu Nigeria, Jama'atu Nasril Islam, JNI, imetangaza kupinga vikali takwa la kupigwa marufuku hijabu nchini humo baada ya baadhi ya magaidi kutumia vazi hilo la stara la kufunika mabomu wanayosheheni mwilini.
Habari ID: 3328801    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/16

Baraza la Kizayuni la mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu limepitisha mpango wa kuyavunjia heshima na kuyabomoa makaburi ya Waislamu katika mji huo.
Habari ID: 3328606    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/15

Waislamu katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa wamemiminika kwa wingi misikitini katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kiasi kwamba baadhi ya barabara zinafungwa kutoa nafasi ziada kwa wanaoswali.
Habari ID: 3325727    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/07

Zaidi ya Waislamu 150 wameuawa katika mashambulio ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram kaskazini mwa Nigeria.
Habari ID: 3322598    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/03

Wazazi Waislamu nchini Kenya wamekosoa kitendo cha uongozi wa shule mbili cha kuwalazimisha wanafunzi wa Kiislamu kuingia makanisani kwa ibada.
Habari ID: 3322404    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/02

Ayatullah Muhsin Araki
Waislamu duniani wametakiwa wasisahau kadhia ya kupigania ukombozi wa Palestina katika kipindi hiki ambapo wengi wanajishughulisha na tatizo sugu la ugaidi na jinai zinazotekelezwa na kundi la kigaidi na kitakifiri la Daesh au ISIS.
Habari ID: 3322212    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/01

Kundi moja la Waislamu wa China wameituhumu serikali ya nchi hiyo kuwa imeanzisha vita visivyo rasmi dhidi ya Waislamu na Uislamu nchini humo.
Habari ID: 3322211    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/07/01

Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani hujuma ya hivi karibuni ya kigaidi dhidi ya msikiti nchini Kuwait.
Habari ID: 3320677    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/28

Waislamu takribani 350,000 wameshiriki katika sala ya Ijumaa ya pili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika msikiti wa Al Aqsa katika Quds Tukufu.
Habari ID: 3320171    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/27

Watu wasiopungua 25wameuawa kufuatia hujuma ya kigaidi iliyolenga msikiti wa Imam Sadiq AS katika mji wa Kuwait.
Habari ID: 3319688    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/26

Waislamu nchini Marekani wamefanya maandamano makubwa kulaani mauaji ya hivi karibuni dhidi ya Wakristo weusi wenye asili ya Afrika ndani ya kanisa moja katika jimbo la Carolina Kusini.
Habari ID: 3317492    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/22

Serikali ya China imepiga marufuku wanafunzi, walimu na watumishi wa umma katika eneo la Xinjiang lenye Waislamu wengi kutekeleza ibada ya Saumu kwenye mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3315931    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/19

Mkuu wa Kamati Kuu ya Kiislamu ya Palestina amewataka Waislamu wahudhurie kwa wingi katika msikiti mtukufu wa al Aqsa wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3314849    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/16

Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa karibu Waislamu nusu milioni wa jamii ya Rohingya huko Myanmar wanaoendelea kukabiliwa na masaibu wanahitaji misaada ya dharura.
Habari ID: 3314114    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/14

Kwa msaada wa Chuo Kikuu cha Minnesota Marekani, wasichana Waislamu katika eneo la Minneapolis wamebuni mavazi mapya ya timu yao ya baskatboli, mavazi ambayo yanazingatia mipaka ya Kiislamu.
Habari ID: 3313760    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/13

Uganda itakuwa mwenyeji wa kikao cha kwanza cha kitaalamu kuhusu ‘Nafasi ya Misimamo ya Wastani ya Kidini Katika Kufikia Ulimwengu Usio na Machafuko’.
Habari ID: 3313360    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/12

Katika jitihada za kueneza mafundisho halisi ya Kiislamu, jumuiya moja ya Kiislamu nchini Nigeria imeanzisha stesheni mpya za televisheni na radio katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.
Habari ID: 3313357    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/06/12

Wajumbe wa Baraza la Uhusiano wa Kiislamu Marekani wameamua kuitisha mkutano na waandishi wa habari katika jimbo la Arizona ili kupambana na vitendo vya kueneza chuki dhidi ya dini hiyo tukufu ya Mwenyezi Mungu.
Habari ID: 3308862    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/05/29

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kuhusu umuhimu wa kuokoa maisha ya wakimbizi wa Myanmar walioachwa baharini kusini mashariki mwa Asia.
Habari ID: 3306970    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/05/24

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea wasiwasi wake kuhusu hatma ya wakimbizi na wahamiaji, wengi wao Waislamu wa kabila la Rohingya kutoka Myanmar, walioachwa kwenye Bahari ya Andaman na Lango la Malakka, kati ya Myanmar, Thailand na Malaysia.
Habari ID: 3305556    Tarehe ya kuchapishwa : 2015/05/19