Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio linaloitaka serikali ya Myanmar kuwapa haki kamili ya uraia Waislamu wa Rohingya.
Habari ID: 2663155 Tarehe ya kuchapishwa : 2015/01/01
Kiongozi mwandamizi wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Uganda Sheikh Ductoor Abdul Qadir Sudi Muwaya aliuawa shahidi Alkhamisi iliyopita. Mkuu wa polisi nchini humo ametangaza kuwa uchunguzi wa kina utafanyika kubainisha aliyetekeleza mauaji hayo.
Habari ID: 2646978 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/29
Mamia ya Waislamu nchini Sweden waliandamana Ijumaa kulaani kitendo cha kushambuliwa msikiti mmoja kwa bomu la petroli siku ya Alkhamisi.
Habari ID: 2637292 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/27
Kutokana na ongezeko kubwa la chuki dhidi ya Waislamu na Uislamu huko Malawi, Waislamu nchini humo wameanzisha kampeni ya kuwashawishi wafuasi wa dini nyinginezo kuzingatia msingi wa ‘kuishi pamoja kwa amani’ ili kuzuia uwezekano wa kuibuka malumbano ya kidini katika nchi hiyo ya kusini wa Afrika.
Habari ID: 2621819 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/18
Waislamu nchini Kenya wanataka vyombo vya habari nchini humo vifanye mabadiliko ya kimsingi kuhusu namna vinavyo tangaza habari kuhusu ugaidi na kuonya kuwa mfumo wa sasa usio wa kitaalamu wa kutangaza habari ni chanzo cha chuki dhidi ya Uislamu katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
Habari ID: 2617613 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/11
Wafanya magendo ya binadamu wanawatumia vibaya wakimbizi Waislamu wanaokimbia mauaji na unyanyasaji wa kuchupa mipaka nchini Myanmar.
Habari ID: 2613658 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/12/01
Imam Khamenei
Ayatullah Udhma Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Jumanne mjini Tehran ameonana na maulamaa, wanavyuoni, wasomi na wageni walioshiriki kwenye Kongamano la Kimataifa la Mirengo ya Kitakfiri kwa Mtazamo wa Maulamaa wa Kiislamu na kulitaja suala la kuzuka upya makundi ya kitakfiri katika miaka ya hivi karibuni kuwa ni tatizo lililopandikizwa na mabeberu katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 2612034 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/26
Waislamu nchini Kenya wamelalamikia vikali hatua ya serikali ya nchi hiyo kufunga misikiti kadhaa katika Kaunti ya Mombasa.
Habari ID: 1476305 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/23
Makundi ya kutetea haki za binadamu yamearifu kuwa, Waislamu wa jamii ya Rohingya wamelazimishwa kuondoka nchini Myanmar katika wiki 3 ziliopita kutokana mpango mpya wa serikali uliozusha mjadala.
Habari ID: 1471524 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/09
Sheikh Bilal Shaaban Katibu Mkuu wa chama cha Hizb Tauhid Islami nchini Lebanon amejiunga na wapenda uhuru na haki duniani katika kulaani vikali hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel kufunga milango ya Msikiti wa Al Aqsa na kuwazuia Waislamu kuswali ndani ya msikiti huo.
Habari ID: 1466340 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/11/01
Misikiti na vituo vya Kiislamu katika mji wa la Inland ndani ya jimbo la California, vimeendelea na juhudi zao za kuwafahamisha watu kuhusu Uislamu wa asili ambao unapenda amani na utulivu.
Habari ID: 1460941 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/17
Katika kipindi cha miaka 23, Mtume Muhammad SAW alisumbuka na kufanya jitihada kubwa mno hadi kuuwezesha kuchipua na kustawi mmea mchanga wa dini tukufu ya Uislamu.
Habari ID: 1459700 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/12
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei ametoa ujumbe wa kila mwaka wa Hija kwa Mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu, ambapo amesema Miongoni mwa masuala muhimu na yanayostahiki kupewa kipaumbele kikubwa zaidi hivi sasa ni suala la mshikamano na umoja wa Waislamu.
Habari ID: 1456588 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/03
Mahujaji takribani milioni tatu wa Nyumba Tukufu ya Allah SWT leo Ijumaa wameanza kutekeleza ibada ya Hijja, ambapo jana usiku walianza kukusanyika katika viwanja vya Arafa nje ya mji mtukufu wa Makka.
Habari ID: 1456586 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/10/03
Mashindano ya Qur’ani yamefanyika nchini Rwanda chini ya himya ya Jumuiya ya Waislamu nchini humo.
Habari ID: 1455972 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/30
Mahakama moja ya Kenya imetoa uamuzi wa kupiga marufuku vazi la Hijabu katika shule moja nchini humo jambo ambalo limewakasirisha sana Waislamu wakiwemo wazazi na wanazuoni wa Kiislamu ambao wameitaja hukumu hiyo kuwa ni hatua nyuma katika uhuru wa kuabudu nchini humo.
Habari ID: 1455483 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/29
Wanazuoni waandamizi wa Kishia na Kisunni nchini Uingereza wamefanya kikao cha pamoja na kujadili njia za kuimarisha umoja miongoni mwa Waislamu sambamba na kukabiliana na kampeni za kuibua fitina katika ulimwengu wa Kiislamu.
Habari ID: 1449625 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/14
Rais Hassan Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sawa na siku za huko nyuma itatumia uwezo wake wote kwa ajili ya kuukomboa mji wa Quds na Msikiti wa Al Aqsa ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu sambamba na kulisaidia taifal linalodhulumiwa la Palestina.
Habari ID: 1445555 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/01
Mufti Mkuu wa Bulgaria ametahadharisha juu ya kuongezeka mashambulio yaliyoratibiwa dhidi ya Waislamu na maeneo ya ibada ya Waislamu katika nchi hiyo ya Ulaya.
Habari ID: 1445545 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/09/01
Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar wangali wanaishi katika hali ngumu na mazingira mabaya na makumi ya maelfu miongoni mwao wanakabiliwa na uhaba wa chakula, maji na huduma za afya.
Habari ID: 1437511 Tarehe ya kuchapishwa : 2014/08/09