chuki dhidi ya uislamu - Ukurasa 12

IQNA

TEHRAN (IQNA)- Serikali ya Uingereza imetakiwa itambue rasmi uwepo wa tatizo la chuki dhidi ya Uislamu yaani Islamophobia ili ikabiliane na tatizo hilo.
Habari ID: 3473786   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/04/05

TEHRAN (IQNA) – Waislamu nchini Ufaransa wamelalamikia hatua ya wakuu wan chi hiyo kupiga marufuku uchinjaji wa kuku kwa misingi ya Kiislamu huku mwezi Mtukufu wa Ramadhani ukikaribia.
Habari ID: 3473749   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/03/20

TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu (Islamophobia) na kusema ubaguzi wa rangi kwa bahati mbaya sana upon a unaendelea katika nchi zote na katika jamii zote duniani na mizizi yake imekita kutokana na karne na karne za ukoloni na utumwa.
Habari ID: 3473747   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/03/19

TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ulimwengu wa Kiislamu una wajibu wa kupambana vilivyo misimamoo mikali ndani yake. Amesema, ni wajibu wa ulimwengu huo kuunganisha nguvu zake kupambana na watu wenye aidiolojia za chuki na za kuwakufurisha Waislamu wengine.
Habari ID: 3473745   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/03/18

TEHRAN (IQNA)- Taasisi za Kiislamu nchini Marekani zimelaani vikali hujuma dhidi ya msikiti unaojengwa mjini Strasbourg.
Habari ID: 3473682   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/02/25

TEHRAN (IQNA)- Bunge la Ufaransa jana Jumanne limeidhinisha sheria iliyo dhidi ya Uislamu na Waislamu nchini humo.
Habari ID: 3473658   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/02/17

TEHRAN (IQNA)- Mwenedo wa chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya hususan nchini Ufaransa ungali unaendelea ambapo Waislamu wa nchi hiyo wamekuwa wakikabiliwa na mashinikizo makubwa.
Habari ID: 3473652   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/02/15

TEHRAN (IQNA) – Zaidi ya hujuma 900 zimeripotiwa dhidi ya Waislamu na taasisi za Kiislamu kote Ujerumani katika mwaka wa 2020.
Habari ID: 3473630   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/02/08

TEHRAN (IQNA)- Wanawake wawili Waislamu waliokuwa wamevaa hijabu walihujumiwa sehemu mbili tafauti Jumatano mjini Edmonton Canada.
Habari ID: 3473628   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/02/06

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi maarufu wa upinzani wa mrengo wa kulia wenye kufurutu ada nchini Ufaransa, Marine Le Pen amependekeza kuwa vazi la Kiislamu la Hijabu lipigwe marufuku kabisa katika maeneo yote ya umma nchini humo.
Habari ID: 3473604   Tarehe ya kuchapishwa : 2021/01/30

TEHRAN (IQNA) -Utawala wa Ufaransa, wenye chuki shadidi dhidi ya Uislamu, umepasisha sheria mpya ya kuzidi kuwabana na kuwakandamiza Waislamu wa nchi hiyo.
Habari ID: 3473446   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/11

TEHRAN (IQNA) -Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani (CAIR), limetangaza kuwa litatenga s ofisi katika makao makuu yake kwa ajili ya kutumiwa na Taasisi ya Kupambana na Chuki Dhidi ya Uislamu au Islamophobia Ufaransa (CCIF) ambayo imefungwa na serikali ya nchi hiyo.
Habari ID: 3473423   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/12/05

TEHRAN (IQNA)- Ikiwa ni katika kuendeleza kampeni dhidi asasi za Kiislamu, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa Gerald Darminian ametangaza mpango wa kupiga marufuku Taasisi ya Kupambana na Chuki Dhidi ya Uislamu au Islamophobia Ufaransa (CCIF).
Habari ID: 3473378   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/20

TEHRAN (IQNA)- Msikiti katika mji wa Zaandam kaskazini magharibi mwa Indonesia umehujumiwa katika jinai ambayo imetajwa kuwa ya wenye chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3473350   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/11

TEHRAN (IQNA)- Wasomi, wanafikra, wanaharakati na wanazuoni wa Kiislamu duniani wametoa wito wa kutungwa sheria zinazozuia kuvunjiwa heshima Mitume wa Mwenyezi Mungu, dini za mbinguni na wafuasi wake.
Habari ID: 3473331   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/05

TEHRAN (IQNA)- Sheikh Mkuu wa al Azhar nchini Misri amekosoa matamshi ya chuki na hujuma ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa dhidi ya Uislamu na kutoa wito wa kutungwa sheria inayotambua chuki na uhasama dhidi ya Waislamu kuwa ni uhalifu.
Habari ID: 3473327   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/11/04

TEHRAN (IQNA)- Baada ya kuchapishwa katuni zinazommvunjia heshima Mtume Muhammad SAW nchini Ufaransa na baada ya hapo matamshi ya Rais Macron wa nchi hiyo kutoa matamshi yenye chuki dhidi ya Uislamu, Waislamu kote duniani wameandamana kulaani vitendo hivyo huku wakiitaka bidhaa za Ufaransa zisusiwe.
Habari ID: 3473305   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/28

TEHRAN (IQNA) – Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau amesema chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) pamoja na misimamo mikali ya mrengo ya kulia ni itikadi ambazo hazina nafasi yoyote katika jamii ya Canada.
Habari ID: 3473260   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/14

TEHRAN (IQNA) - Waislamu wa Ufaransa wameudhika kwa kauli za chuki dhidi ya Uislamu zilizotolewa na rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron.
Habari ID: 3473226   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/10/03

Waziri Mkuu wa Pakistan
TEHRAN (IQNA)- Waziri Mkuu wa Pakistan ametoa wito kwa Umoja wa Mataifa kuunda muungano wa kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu au Islamophobia.
Habari ID: 3473203   Tarehe ya kuchapishwa : 2020/09/26