iqna

IQNA

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, utawala wa Marekani ni nembo ya ushari, utumiaji mabavu, kuanzisha migogoro na kuzusha vita.
Habari ID: 3471834    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/02/09

TEHRAN (IQNA)- Katika wakati huu wa kukaribia maadhimisho ya miaka 40 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei mapema leo asubuhi mjini Tehran amefanya ziara katika Haram toharifu ya Imam Khomeini MA, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu na mbali na kuswali katika Haram hiyo na kumsomea Faatiha, amemuombea dua za kheri mwanachuoni huyo mkubwa wa zama hizi.
Habari ID: 3471825    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/01/30

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametilia mkazo kuutazama kila mara kwa jicho baya ushauri wa Wamagharibi, na akafafanua kwa kusema: Nchi za Magharibi, ambazo leo hii zimepata maendeleo mengi katika elimu na sayansi mpya, zimetenda jinai nyingi pia dhidi ya mataifa katika zama zote za historia.
Habari ID: 3471817    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/01/24

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria kuendelea kudhoofika mpaka leo vyombo vya mikakati na mahesabu vya Marekani ni ukweli halisi wa mambo na akafafanua kwa kusema: "Baadhi ya viongozi wa Marekani hujifanya na hutaka waonekane wendawazimu, tab'an mimi hili sikubaliani nalo, lakini lililo hakika, wao ni "wapumbavu wa daraja la kwanza".
Habari ID: 3471802    Tarehe ya kuchapishwa : 2019/01/10

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Palestina itaendelea kuwa taifa lenye nguvu na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, katika kipindi kisicho mbali sana taifa hilo litaweza kupata ushindi wa mwisho.
Habari ID: 3471792    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/31

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullahil Udhma Ali Khamenei leo asubuhi ameongoza Swala ya maiti ya marhumu ya Ayatullah Mahmoud Hashemi Shahroudi, aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Iran.
Habari ID: 3471787    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/26

TEHRAN (IQNA) – Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia zimesaini Mapatano ya Maelewano (MOU) kuhusu kushiriki Wa iran i katika ibada ya Hija mwaka huu wa 1440 Hijria na 2019 Miladia.
Habari ID: 3471777    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/19

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, maadui wamefeli katika njama ya maadui wa Iran ya kuwachoche baadhi ya watu kufanya maandamano mitaani na kuyapa jina la "Majira ya Joto Kali".
Habari ID: 3471769    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/13

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) -Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa umoja, mshikamano na kauli moja ya ulimwengu wa Kiislamu vitazishinda njama za maadui.
Habari ID: 3471752    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/11/26

Kiongozi wa Hamas
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amehutubu katika Kongamano la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu mjini Tehran na kusema: "Utawala wa Kizayuni ni adui mkuu wa Umma wa Kiislamu."
Habari ID: 3471750    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/11/24

TEHRAN (IQNA) - Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madehehbu za Kiislamu amesema wanazuoni, wanaharakati wa kisiasa na wasomi kutoka nchi 100 wamealikwa kushiriki katika Kongamano la 32 la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu ambalo limepangwa kufanyika mjini Tehran.
Habari ID: 3471743    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/11/17

TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amewapongeza wanamichezo wa kike Wa iran i ambao wanashiriki katika michezo ya kimataifa wakiwa wamevaa vazi la staha la Hijabu.
Habari ID: 3471741    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/11/14

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, kudidimia nguvu na uwezo wa Marekani ni ukweli ambao wataalamu duniani wameafiki.
Habari ID: 3471727    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/11/03

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, majimui kubwa ya vijana wa nchi na taifa kubwa la Iran litaushinda wenzo wa mwisho wa adui yaani vikwazo na kutoa kipigo kingine dhidi ya Marekani.
Habari ID: 3471701    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/10/04

TEHRAN (IQNA)- Qarii (msomaji wa Qur'ani) ameibuka mshindi katika Mashindano ya 25 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Croatia yaliyomalizika Jumamosi.
Habari ID: 3471697    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/09/30

Rais Rouhani akihutubu katika Umoja wa Mataifa
TEHRAN (IQNA)-Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya lran amesema Marekani ilikiuka sheria kinyume na misingi na sheria za kimataifa kwa kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran yaliyoidhinishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Habari ID: 3471691    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/09/26

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullha Sayyed Ali Khamenei ametuma salamu za rambirambi kwa familia za mashahidi wa tukio chungu la hujuma ya kigaidi katika mji wa Ahvaz kusini mwa Iran leo asubuhi.
Habari ID: 3471686    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/09/22

Kiongozi Muadhamu katika mkutano na rais wa Uturuki
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema hitajio muhimu zaidi katika ulimwengu wa Kiislamu hii leo ni ukuruba zaidi na mshikamano wa nchi za Kiislamu.
Habari ID: 3471662    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/09/07

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria matamashi na lugha zisizo na adabu za viongozi wa Marekani kuhusiana na vikwazo, vita na mazungumzo na Iran kusema kuwa, tunasisitiza kwamba, hakutatokea vita na hatutafanya mazungumzo.
Habari ID: 3471628    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/08/13

TEHRAN (IQNA) Imran Khan, Mkuu wa chama cha Tehreek-e-Insaf (PTI) cha nchini Pakistan na kilichoshinda uchaguzi wa Bunge la nchi hiyo amesisitiza kuwa chama chache kinataka kustawisha uhusiano mwema na maj iran i zake ikiwemo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3471609    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/07/27