Mkuu wa Kituo cha Masuala ya Qur'ani cha Shirika la Wakfu na Misaada Hamid Majidimehr, Naibu wa Baraza Kuu la Qur'ani Mohammad Taqi Mirzajani, na mkuu wa msafara huo Ali Salehi Matin pia walihudhuria mkutano huo.
Mirzajani alisema katika kikao hicho kuwa msafara huo utakaa Saudi Arabia kwa takriban siku 40 na utarejea nchini mapema mwezi Julai.
Majidimehr pia alihutubia mkutano huo, akisema wanachama wa msafara wanapaswa kujitahidi kufanya vyema katika safari hiyo ya kiroho na kutimiza majukumu yao ipasavyo.
Kuweza kuhiji na kwenda kwenye ardhi ya wahyi kama mjumbe wa msafara wa Qur'ani ni uzoefu wa kipekee, alisema.
Kila mwaka mamilioni ya Waislamu kutoka duniani kote hukusanyika Makka kwa ajili ya Hija ya kila mwaka. Iran pia inatuma mahujaji pamoja na makundi ya wanaharakati wa Qur'ani, wanaojulikana kama Msafa Nur wa Hija. Wajumbe wa ujumbe huo wana programu za Qur'ani, ikiwa ni pamoja na vikao vya kusoma Qur'ani kwa mahujaji katika miji mitakatifu ya Makka na Madina.
3488122