Mchakato wa mazishi ya Shahidi Nasrallah na afisa mwingine mkuu wa Hizbullah, Shahidi Sayed Hashem Safieddine, unatarajiwa kufanyika Jumapili kuanzia saa saba adhuhuri kwa saa za eneo hilo.
Wawakilishi rasmi kutoka Yemen, Iraq, Tunisia, Iran, Mauritania, na Uturuki ni miongoni mwa wageni wa kimataifa ambao wamewasili Lebanon kwa ajili ya tukio hilo.
Kamati iliyoundwa kuandaa mazishi hayo ilisema katika taarifa yake siku ya Ijumaa kwamba wapenda uhuru kutoka kote ulimwenguni wameanza safari yao kuelekea Beirut, na idadi ya washiriki ni kubwa kiasi kwamba mitaa haitatosha kuwaweka wote kwa siku moja.
Kadri siku ya mazishi inavyokaribia, vyanzo vya Iraq vinavyoripoti kwamba ndege kutoka Baghdad kwenda Beirut zimejaa, na mashirika ya ndege yanaongeza idadi ya safari za ndege.
Sehemu kuu ya mchakato wa mazishi itafanyika kwenye uwanja wa michezo na Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sheikh Naim Qassem, atahutubia tukio hilo.
Aidha, viwanja vyote vya Beirut vimewekwa na skrini kubwa kwa watu kufuatilia sherehe na kusikiliza hotuba ya Sheikh Qassem.
Nasrallah aliuawa shahidi tarehe 27 Septemba 2024, katika shambulio la kigaidi la anga la utawala haramu wa Israel kwa kutumia mabomu yanayotengenezwa na Marekani. Naye Sayyid Safieddine pia aliuawa shahidi katika shambulio la kigaidi la Israel mwezi wa Oktoba mwaka jana pia.
3491959