IQNA

Wageni wa kimataifa wawasili Beirut kwa mazishi ya Shahidi Nasrallah

21:47 - February 22, 2025
Habari ID: 3480255
IQNA – Wageni rasmi na wasio rasmi kutoka nchi mbalimbali wamewasili katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut, kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa katibu mkuu wa Hizbullah, Sayed Hassan Nasrallah.

Mchakato wa mazishi ya  Shahidi Nasrallah na afisa mwingine mkuu wa Hizbullah, Shahidi Sayed Hashem Safieddine, unatarajiwa kufanyika Jumapili  kuanzia saa saba adhuhuri kwa saa za eneo hilo.

Wawakilishi  rasmi kutoka Yemen, Iraq, Tunisia, Iran, Mauritania, na Uturuki ni miongoni mwa  wageni wa kimataifa ambao wamewasili Lebanon kwa ajili ya tukio hilo.

Kamati iliyoundwa kuandaa mazishi hayo ilisema katika taarifa yake siku ya Ijumaa kwamba wapenda uhuru kutoka kote ulimwenguni wameanza safari yao kuelekea Beirut, na idadi ya washiriki ni kubwa kiasi kwamba mitaa haitatosha kuwaweka wote kwa siku moja.

Kadri siku ya mazishi inavyokaribia, vyanzo vya Iraq vinavyoripoti kwamba ndege kutoka Baghdad kwenda Beirut zimejaa, na mashirika ya ndege yanaongeza idadi ya safari za ndege.

Sehemu kuu ya mchakato wa mazishi itafanyika kwenye uwanja wa michezo na Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sheikh Naim Qassem, atahutubia tukio hilo.

Aidha, viwanja vyote vya Beirut vimewekwa na skrini kubwa kwa watu kufuatilia sherehe na kusikiliza hotuba ya Sheikh Qassem.

Nasrallah aliuawa shahidi tarehe 27 Septemba 2024, katika shambulio la kigaidi la anga la utawala haramu wa Israel kwa kutumia mabomu yanayotengenezwa na Marekani. Naye Sayyid Safieddine pia aliuawa shahidi katika shambulio la kigaidi la Israel mwezi wa Oktoba mwaka jana pia.

3491959

Habari zinazohusiana
captcha