
Sheikh Ali Umar Yaqoub Abbasi alitoa shukrani zake kwa serikali na wananchi wa Malaysia kwa dua zao zisizokatika na msaada wa kibinadamu unaoendelea kwa watu wa Palestina, ndani ya Gaza na Al-Quds.
Waziri Mkuu wa Malaysia, Anwar Ibrahim, alisema kuwa shukrani hizo ziliwasilishwa kwake binafsi na Sheikh Ali Umar wakati wa kikao kilichofanyika Jumatatu. Katika mazungumzo hayo, pande zote mbili walishirikiana maoni na kukubaliana juu ya umuhimu wa kulinda utukufu wa Msikiti wa Al-Aqsa pamoja na mustakabali wa Al-Quds.
Anwar Ibrahim aliongeza: “Nimeeleza pia juhudi zinazotekelezwa na Serikali ya Kuala Lumpur kuendeleza msaada wa kulinda na kuikomboa Al-Aqsa. Mwenyezi Mungu (SWT) aendelee kubariki juhudi zetu tunaposimama bega kwa bega na ndugu zetu Wapalestina kupinga ugaidi wa utawala wa Kizayuni wa Israel.”
Katika kikao hicho pia alihudhuria Waziri wa Mambo ya Dini wa Malaysia, Zulkifli Hassan.
3495982