IQNA

ICRO imeandaa Tuzo ya Kimataifa ya Arbaeen Toleo la 12

17:07 - July 13, 2026
Habari ID: 3482480
IQNA – Shirika la Iran la Utamaduni na Uhusiano wa Kiislamu (ICRO) limeandaa tuzo ya 12 ya Kimataifa ya Arbaeen mwaka huu.

Tuzo hiyo imeandaliwa kwa lengo la kueneza ujumbe wa Arbaeen duniani kote na kuonyesha misingi ya kiongozi mtaratibu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei aliyeuawa shahidi, ambaye alikuwa mfanyaziara wa kwanza wa Arbaeen mwaka huu.

Kwa mujibu wa ofisi ya uhusiano wa umma ya ICRO, kwa kutegemea urithi wa kudumu wa Kiongozi Shahidi, ICRO imetumia utukufu wa kipekee wa Arbaeen kuwa uwanja wa kueneza ukweli kupitia tuzo ya kimataifa.

ICRO imebainisha kuwa hatua hii ni mwitikio wa hitaji la kulinda njia iliyoachwa na kiongozi aliyefariki shahidi wakati wa mzunguko wa Arbaeen, ambao umevuka mipaka na kuwa ustaarabu wa kimataifa.

Nyanja za tuzo hii ya 12 ya Kimataifa ya Arbaeen zinajumuisha: picha, filamu, simulizi za safari na kumbukumbu, ushairi, nyimbo za Arbaeen, na wanaharakati wa mtandao.

Katika mwaka huu ambapo kivuli cha kutokuwepo kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Khamenei (RA), kimegusa kwa uzito mwili wa Umma wa Kiislamu na ulimwengu kwa ujumla, ICRO inaona jukumu lake la kuelezea ukweli wa safari hii ya kiroho kuwa kubwa mara mbili.

Kwa sababu hiyo, toleo la 12 la Tuzo ya Kimataifa ya Arbaeen linajumuisha tuzo maalum kwa kuzingatia mada za: “Uimara wa Imam aliyefariki shahidi, na utume wa watu wema” pamoja na “Dhuluma dhidi ya watoto waliofariki shahidi wa Minab, na ushujaa wa wapiganaji jasiri.”

Tarehe ya mwisho ya kuwasilisha kazi kwa ajili ya toleo hili ni tarehe 1 Novemba, 2026. Wale wenye nia wanaweza kuwasilisha kazi zao kupitia tovuti rasmi ya Tuzo ya Kimataifa ya Arbaeen.

Tuzo ya Kimataifa ya Arbaeen ya mwaka huu si tukio la kuwaenzi washindi pekee; bali ni mwitikio wa makusudi kwa hitaji la ulimwengu la kusoma upya ujumbe wa ujenzi wa ustaarabu wa Arbaeen chini ya mwongozo wa kudumu wa Imam aliyefariki shahidi wa Mapinduzi.

ICRO, ikiwa ni chombo cha diplomasia ya umma cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, inajaribu kujenga daraja kati ya mafundisho matakatifu ya Arbaeen na hitaji la kulinda njia iliyochorwa na Kiongozi wa Umma aliyefariki shahidi. Kwa kuandaa tuzo hii, ICRO inategemea urithi wa kiroho na mafundisho ya kimkakati ya kiongozi huyo, na kurejesha roho ile ile ya upinzani (resistance) kupitia kazi za kitamaduni na kisayansi. Lengo ni kuthibitisha kuwa ingawa Kiongozi amefariki shahidi, njia yake bado inaishi na imara ndani ya mioyo ya kila mtafutaji na kila mjumbe wa ukweli.

Kila mwaka, Tuzo ya Kimataifa ya Arbaeen huwakutanisha kazi za kibunifu katika nyanja za utamaduni, sanaa, na vyombo vya habari vinavyohusiana na mahujaji wa Arbaeen kutoka sehemu mbalimbali za ulimwengu.

Arbaeen, huadhimisha siku 40 baada ya Siku ya Ashura (tarehe 10 Muharram), ambayo huomboleza kuuawa kwa shahidi, Imam Hussein (AS), mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW). Katika kalenda ya mwezi ya Kiislamu, siku hii huangukia tarehe 20 Safar. Misafara ya ziara ya Arbaeen huanza kabla ya tarehe hiyo.

/3498235

captcha