waislamu - Ukurasa 49

IQNA

TEHRAN (IQNA) – Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ametoa hakikisho kuwa, Waislamu watakaofariki nchini humo kutokana na ugonjwa wa COVID-19 au corona watazikwa kwa mujibu wa taratibu za Kiislamu.
Habari ID: 3472648    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/09

TEHRAN (IQNA) – Baraza la Maulamaa Russia limetangaza Fatwa mpya inayowataka Waislamu waswali katika majumba yao katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika mwaka huu wa 1441 Hijria Qamaria ili kuzuia kuenea zaidi ugonjwa ambukizi wa COVID-19 au corona.
Habari ID: 3472647    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/09

Janga la Corona
TEHRAN (IQNA) – Pakistan imewaweka katika karantini watui 20,000, na inawasaka maelifu yaw engine, walioshiriki katika mjumuiko wa Waislamu ambao ni maarufu kama Ijtimai katika mji wa Lahore mwezi uliopita, huku janga la COVID-19 au corona likiendelea kuwa mbaya nchini humo.
Habari ID: 3472646    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/08

TEHRAN (IQNA) – Mkuu wa Idara ya Hija na Ziyara ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameelezea matumaini yake kuwa, janga la COVID-19 au corona litamalizika utakapowadia msimu wa joto na kwamba Hija itafanyika kama ilivyopangwa. Hatahivyo ameongeza kuwa, Iran iko tayari kwa hali yoyote itakayojitokeza kuhusu Ibada ya Hija mwaka huu.
Habari ID: 3472643    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/07

TEHRAN (IQNA) – Makundi ya wabaguzi wenye misimamo mikali wa mrengo wa kulia yanatumia janga la ugonjwa wa COVID-19 au corona kueneza chuki dhidi ya Waislamu nchini Uingereza.
Habari ID: 3472640    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/06

TEHRAN (IQNA)- Wizara ya Wakfu nchin Misri imetangaza kuwa ni marufuku kuandaa futari kwa umma misikitini katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3472635    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/05

TEHRAN (IQNA) – Ugonjwa wa COVID-19 au corona umepelekea kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu nchini India.
Habari ID: 3472631    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/04

Hofu ya corona
TEHRAN (IQNA) – Saudi Arabia imetangaza sheria kali ya kutotoka nje katika miji mitakatifu ya Makka na Madina ikiwa ni sehemu za mkakati wa utawala huo wa kifalme kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19 au corona.
Habari ID: 3472627    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/04/02

TEHRAN (IQNA) – Serikali ya Kuwait imetangaza mpango wa kuanzisha masoo ya kuhifadhi Qur'ani kupitia intaneti baada ya madrassah za Qur'ani nchini humo kufungwa kwa muda ili kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama kirusi cha corona.
Habari ID: 3472600    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/25

TEHRAN (IQNA) – Uongjwa wa COVID-19 maarufu kama corona umewaathiri Waislamu kote duniani hasa kutokana na kufungwa misikiti kwa muda ili kuzuia kuenea ugonjwa huo na hivi sasa viongozi wa Kiislamu wanabadilisha mbinu za kuwaongoza Waislamu kiroho.
Habari ID: 3472597    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/24

TEHRAN (IQNA) – Misikiti kadhaa muhimu katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi imefungwa kutokana na hofu ya kuenea ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama kirusi cha corona.
Habari ID: 3472580    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/19

TEHRAN (IQNA) – Baadhi ya misikiti katika mji wa Cape Town Afrika Kusini imetangaza kufunga milango yake kwa muda ili kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19 au corona.
Habari ID: 3472579    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/18

TEHRAN (IQNA) – Harakati zote misikitini nchini Malayasia, ikiwa ni pamoja na sala za Ijumaa, zimesitishwa kwa muda wa siku kumi kufuatiia amri ya mfalme wa nchi hiyo ili kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama kirusi cha corona.
Habari ID: 3472574    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/17

TEHRAN (IQNA) - Utawala wa Kizayuni wa Israel umemkamata Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Wakfu wa Kiislamu katika mji wa Quds (Jerusalem) huku kukiwa na tetesi kuwa Wazayuni wanalenga kumuambukjiza kirusi cha corona.
Habari ID: 3472571    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/16

TEHRAN (IQNA)- Serikali ya Kuwait imefunga kwa muda misikiti nchini na kubadilisha adhana kufuatia hofu ya kuenea ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama corona.
Habari ID: 3472570    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/16

TEHRAN (IQNA)- Bunge la Uingereza, House of Commons, litaanza kuuza chakula Halali, ambacho kimetayarishwa kwa misingi ya mafundisho ya Kiislam, kuanzia Machi 30 kufuatia ombi la wabunge Waislamu.
Habari ID: 3472568    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/15

TEHRAN (IQNA) - Jumuiya ya Kimataifa ya Mwamko wa Kiislamu imelaani mauaji yanayofanywa ma Wahindu wenye misimamo mikali dhidi ya Waislamu nchini India na kuitaka serikali ya nchi hiyo isitishe mauaji na jinai hiyo.
Habari ID: 3472559    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/13

TEHRAN (IQNA) - Vyombo vya habari vya Ufaransa vimetangaza kuwa, jana usiku mtu mmoja mwenye silaha alishambulia msikiti mmoja mjini Parisa.
Habari ID: 3472548    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/09

TEHRAN (IQNA) – Wakuu wa Saudi Arabia Jumatatu Jumatatu wametangaza kusitisha shughuli zote za usomaji Qur'ani na mafundisho mengine misikitini kufuatia hofu ya kuenea ugonjwa wa COVID-19 maarufu kama Corona.
Habari ID: 3472546    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/09

TEHRAN (IQNA)- Ayatullah Nouri Hussein Hamedani ambaye ni miongoni mwa viongozi wa juu wa kidini nchini Iran amelaani ukatili na mauaji yanayoendelea kufanywa dhidi ya Waislamu nchini India na kukosoa kimya cha vyombo vya habari duniani kuhusiana na mauaji hayo.
Habari ID: 3472540    Tarehe ya kuchapishwa : 2020/03/07