TEHRAN (IQNA) – Shirika la Ndege la Delta Airlines la Marekani limetozwa faini ya dola 50,000 kwa kuwatimua wasafiri watatu Waislamu ambao tayari walikuwa wameshapanda ndege hata baada ya maafisa wa usalama kusema hakukuwa na tatizo lolote la usalama.
Habari ID: 3472407 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/26
TEHRAN (IQNA) - Brigedi za Hizbullah ya Iraq zimesema kuwa mapinduzi ya wananchi wa nchi hiyo yataendelea hadi wavamizi wote wa Kimarekani watakapofurushwa kikamilifu nchini Iraq na katika eneo zima la Asia Magharibi.
Habari ID: 3472405 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/25
Hujjatul Islam Walmuslimin Sayyid Muhammad Hassan Abu Turabi-Fard
TEHRAN (IQNA) - Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran amesema kuwa mauaji yaliyofanywa na jeshi la kigaidi la Marekani dhidi ya Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Luteni Jenerali Qassem Soleimani ni mwanzo wa kufukuzwa Marekani katika eneo hili la magharibi mwa Asia sambamba na washirika wake katika eneo kusambaratika.
Habari ID: 3472403 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/24
TEHRAN (IQNA) – Watu wa matabaka mbali mbali nchini Afrika Kusini wamekusanyika mbele ya Ubalozi wa Marekani mjini Pretoria kulaani sera za Rais Trump wa Marekani dhidi ya Iran.
Habari ID: 3472400 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/23
TEHRAN (IQNA) – Baraza la Shura (Mashauriano) la Jumuiya ya Waislamu Uingereza limemchagua Bi. Raghad Al Tikriti kuwa mwenyekiti wake mpya.
Habari ID: 3472398 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/23
TEHRAN (IQNA) - Wanajeshi katili wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi kwa kuwapiga risasi Wapalestina watatu katika uzio wa Ukanda wa Ghaza.
Habari ID: 3472396 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/22
TEHRAN (IQNA) – Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani (CAIR) limeanzisha kampeni maalumu ya kuwahimiza Waislamu kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa rais utakaofanyika nchini humo mwaka 2020.
Habari ID: 3472395 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/22
TEHRAN (IQNA) – Awamu ya kwanza ya ukarabati muhimu wa Msikiti wa Al Nouri mjini Mosul Iraq imekamilika. Msikiti huo ulihujumiwa na kubomolewa na kundi la kigaidi la ISIS (Daesh) mwaka 2017.
Habari ID: 3472394 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/22
TEHRAN (IQNA)- Misri imeandaa hafla ya kumbukumbu ya kuzaliwa qarii mashuhuri wa Qur'ani Tukufu nchini humo Mohamed Siddiq El-Minshawi.
Habari ID: 3472392 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/21
TEHRAN (IQNA) – Kasisi Mkristo ambaye alikuwa anasikiliza qiraa ya Qur'ani Tukufu nchini Misri alivutiwa sana na usomaji huo na akatoa shukrani zake kwa kumkumbatia.
Habari ID: 3472388 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/20
TEHRAN (IQNA) – Mbunge katika chama tawala chenye misimamo mikali ya Kihindu cha Bharatiya Janata (BJP) nchini India ametishia kuwa, misikiti iliyojengwa katika 'ardhi ya serikali' katika mji wa New Delhi itabomolewa.
Habari ID: 3472386 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/19
TEHRAN (IQNA) – Serikali mpya ya mseto nchini Austria imekosolewa kutokana na kufuata sera dhidi ya Waislamu na raia wa kigeni.
Habari ID: 3472377 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/16
TEHRAN (IQNA) – Msikiti wa Quebec Canada unaendelea kukarabatiwa ili kuwawezesha Waislamu wa mji huo kupata eneo salama la ibada.
Habari ID: 3472376 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/16
TEHRAN (IQNA) – Waumini wanarejea katika misikiti mitano ya kihistoira ambayo imekarabatiwa na kuanza kutumiwa baada ya hadi miongo sita.
Habari ID: 3472375 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/15
TEHRAN (IQNA) – Harakati ya Kiislamu ya Nigeria imetoa taarifa kulalimikia hatua ya utawala wa nchi hiyo kuendelea kumshikilia korokoroni kiongozi wa harakati hiyo Sheikh Ibrahim Zakzaky.
Habari ID: 3472374 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/15
TEHRAN (IQNA) - Waislamu wa Ivory Coast wamefanya kikao cha kumuenzi na kumkumbuka Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na mashahidi wenzake waliouawa hivi karibuni na askari magaidi wa Marekani nchini Iraq.
Habari ID: 3472373 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/15
TEHRAN (IQNA) – Mwenyekiti wa Baraza la Kiislamu Malaysia (MAPIM) amesema hatua ya Marekani ya kumuua kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Luteni Jenerali Qassem Soleimani ni ugaidi wa kiserikali na ukweli wa mambo ni kuwa Rais Donald Trump wa Marekani ni muuaji.
Habari ID: 3472372 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/14
TEHRAN (IQNA) – Kampeni mpya imezinduliwa huko mjini Dallas, Marekani kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu misingi ya mafundisho ya Kiislamu.
Habari ID: 3472371 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/14
TEHRAN (IQNA) - Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani (CAIR) limekosoa ujumbe wa Twitter wa Rais Donald Trump wa nchi hiyo wenye kukejeli Uislamu na Waislamu na kusema ujumbe huo unaweza kuhatarisha maisha ya Wamarekani Waislamu na Masingasinga.
Habari ID: 3472370 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/14
TEHRAN (IQNA) - Shirika la Ushirikkiano wa Nchi za Kiislamu (OIC) limelaani vikali hujuma ya bomu ambayo ililenga msikiti huko Quetta, Pakistan na kupelekea watu kadhaa kuuawa na kujeruhiwa.
Habari ID: 3472368 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/01/13