TEHRAN (IQNA) - Aya za Qur'ani Tukufu zimesomwa katika Kanisa Kubwa la Hagia Sophia ambalo sasa ni jumba la makumbusho mjini Istanbul Uturuki.
Habari ID: 3472812 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/29
TEHRAN (IQNA) – Wizara ya Wakfu ya Syria imetangaza kuanza swala za jamaa katika misikiti ya nchi hiyo kuanzia sikua ya Jumatano.
Habari ID: 3472808 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/27
TEHRAN (IQNA) – Mwakilishi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini India amesisitiza umuhimu wa Waislamu kudumisha mafanikio waliyoweza kuyapata katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3472804 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/26
TEHRAN (IQNA) – Siku kuu ya Idul Fitr ni kati ya siku kuu muhimu zaidi katika ulimwengu wa Kiislamu na kawaida huwa siku ya mapumziko. Mwaka huu katika aghalabu ya nchi za Kiislamu kumekuwa na hali maalumu ya tahadhari wakati wa Idi ili kuzuia kuenea ugonjwa wa corona.
Habari ID: 3472799 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/25
TEHRAN (IQNA) - Rais Frank-Walter Steinmeier wa Ujerumani sambamba na kutoa pongezi kwa mnasaba wa Sikukuu ya Idul-Fitr, ametaka wananchi wote washirikiane kwa ajili ya kuwalinda Waislamu wa nchi hiyo.
Habari ID: 3472798 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/24
TEHRAN (IQNA)- Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia viongozi wa nchi za Kiislamu na Waislamu kote duniani salamu za kheri na fanaka kwa mnasaba wa kuwadia siku kuu ya Idul Fitr.
Habari ID: 3472795 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/24
TEHRAN (IQNA)- Jaji wa kwanza Muislamu mwenye kuvaa Hijabu ameteuliwa katika mfumo wa mahakama nchini Uingereza.
Habari ID: 3472794 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/23
Sayyid Hassan Nasrallah
TEHRAN (IQNA) - Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema hakuna shaka kuwa utawala wa Israel utasambaratika na amesisitiza kuwa, vita asili vitakuwa na Marekani.
Habari ID: 3472793 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/23
TEHRAN (IQNA) – Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, ameutahadharisah vikali utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kuchukua hatua zozote dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem).
Habari ID: 3472787 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/21
Rais Hassan Rouhani wa Iran
TEHRAN (IQNA) - Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria kukaribia maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds na kusisitiza kuwa, Quds (Jerusalem) katu haitasahauliwa na haitaendelea kubakia katika uvamizi wa madhalimu.
Habari ID: 3472785 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/20
TEHRAN (IQNA) – Kila mwaka kwa kuanza Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, familia za wenyeji wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) au Imarati hujumuika pamoja zaidi ya wakati wowote mwingine katika makwa.
Habari ID: 3472782 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/19
TEHRAN (IQNA) – Utawala wa jimbo la Java Mashariki nchini Indonesia umebatilisha idhini ya Sala ya Idul Fitr katika Msikiti wa Al Akbar mjini Surabaya baada ya wataalamu kuonya kuhusu matokeo mabaya ya mjumuiko wa watu wengi wakati wa kipindi hiki cha janga la COVID-19.
Habari ID: 3472780 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/19
TEHRAN (IQNA)- Sheikh Bujuma Albaz, Imamu na Khatibu katika Msikiti wa Mohammad wa Sita katika mji wa Bouznika ana sauti nzuri na yenye mvuto ya kusoma Qur'ani yenye kushabihiana na ile ya qarii mashuhuri wa Misri Abdul Basit Abdul Swamad.
Habari ID: 3472778 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/18
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) - Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, kuwasha moto wa vita katika nchi kadhaa ikiwemo Afghanistan, Iraq na Syria ni miongoni mwa sababu za kuchukiwa Marekani na akabainisha kwamba, Wamarekani wanaeleza kinagaubaga kuwa 'tumeweka vikosi Syria kwa sababu kuna mafuta'; lakini bila shaka hawataweza kubaki, si Iraq wala Syria. Ni lazima waondoke huko na hakuna shaka kuwa wataondoshwa tu.
Habari ID: 3472777 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/18
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Siku ya Kimataifa ya Quds itaadhimishwa nchini Iran na pia Swala ya Idul FItr itaswaliwa kwa kuzingatia kanuni za afya kuhusiana na ugonjwa wa COVID-19.
Habari ID: 3472770 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/16
TEHRAN (IQNA) – Tokea mwaka 1975, Wakristo nchini Misri wamekuwa wakiwatayarishia Waislamu futari katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3472769 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/15
TEHRAN (IQNA) - Wizara ya Mambo ya Nje Iran imetoa tamko kuhusu siku ya "Nakba" yaani siku ya nakama ya kuasisiwa utawala pandikizi wa Kizayuni katika ardhi walizoporwa Wapalestina na kusisitiza kuwa, kadhia ya Palestina itaendelea kuwa suala kuu nambari moja katika ulimwengu wa Kiislamu licha ya kufanyika njama nyingi za kulisahaulisha.
Habari ID: 3472767 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/15
TEHRAN (IQNA) – Misikiti nchini Italia itaendelea kufungwa wakati wa Sala ya Idul Fitri ikiwa ni katika muendelezo wa kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19.
Habari ID: 3472765 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/14
TEHRAN (IQNA) – Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni mwezi wa Ibada ambao huwajumuisha Waislamu kwa lengo moja.
Habari ID: 3472764 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/14
TEHRAN (IQNA) – Misikiti ya London Mashariki nchini Uingereza imeanza kuadhini kupitia vipaza sauti katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili kuwasaidia Waislamu wajihisi kufungamana na misikiti ambayo imefungwa kwa muda kuzuia kuenea ugonjwa wa COVID-19.
Habari ID: 3472752 Tarehe ya kuchapishwa : 2020/05/10