waislamu - Ukurasa 76

IQNA

TEHRAN (IQNA)-Mufti mkuu wa Libya amelaani vikali namna utawala wa kifalme Saudia unavyowakandamiza wanazuoni wa Kiislamu.
Habari ID: 3471383    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/02/07

TEHRAN (IQNA)-Mahakama moja nchini Ujerumani imepiga marufuku adhana kwa kutumia vipaza sauti katika msikiti moja kwa madai kuwa eti wasiokuwa Waislamu wanakerwa.
Habari ID: 3471382    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/02/06

TEHRAN (IQNA)-Serikali ya Uganda imeidhinisha sheria za mfumo wa benki za Kiislamu huku benki kuu nchini humo ikitazamiwa kuchapisha rasmi sheria hizo kama sehemu ya mikakati ya kuwashirikisha Waislamu kikamilifu katika mfumo wa kifedha.
Habari ID: 3471381    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/02/05

TEHRAN (IQNA)-Watu wasiojulikana wameuhujumu na kuharibu msikiti katika mji wa The Hague nchini Uholanzi.
Habari ID: 3471380    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/02/04

TEHRAN (IQNA)- Utawala wa Aal Khalifa nchini Bahrain unaendelea kutekeleza sera za ukandamizaji dhidi ya wapinzani ikiwa ni pamoja na kuwanyonga, kuwatesa, kuwapokonya uraia na kuwalazimui kuihama nchi huku mashirika ya kutetea haki za binadamu yakinaani uovu huo ambao umenyamaziwa kimya na Umoja wa Mataifa na nchi za Magharibi.
Habari ID: 3471379    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/02/03

TEHRAN (IQNA)-Makaburi ya umati ya Waislamu waliouawa nchini Myanmar yamepatikana katika kijiji kimoja katika jimbo la Rakhine magharibi mwa nchi hiyo.
Habari ID: 3471378    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/02/02

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amebainisha masikitiko yake makubwa kutokana na kuuawa watu wasio na hatia katika hujuma za hivi karibuni za kigaidi nchini Afganistan na kusema: "Lengo la Marekani katika kuhamishia Afghanistan magaidi wa ISIS (Daesh) ni kuhalalisha uwepo wake katika eneo sambamba na kudhamini usalama wa utawala wa Kizayuni."
Habari ID: 3471376    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/30

TEHRAN (IQNA)-Nchi za Kiislamu zilizo na uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel zimetakiwa zikate uhusiano huo mara moja kama njia ya kuunga mkono ukombozi wa Palestina hasa mji wa Quds (Jerusalem).
Habari ID: 3471375    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/29

Waziri wa Mambo ya Ndani Pakistan
TEHRAN (IQNA)-Waziri wa Mambo ya Ndani Pakistan Ahsan Iqbal amesema Qur'ani Tukufu ni kama ramani ya njia katika mwaisha ya mwanadamu.
Habari ID: 3471374    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/28

TEHRAN (IQNA)-Waislamu zaidi ya 100,000 kutoka jamii ya Uighur nchini China wanasemekana kushikiliwa kwa nguvu katika kambi zenye msongamano mkubwa ambapo wanafunzwa itikadi za Kikomunisti.
Habari ID: 3471373    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/27

TEHRAN (IQNA)-Nakala nne nadra za Qur'ani Tukufu ni kati ya turathi zenye thamani katika maktaba ya Msikiti wa Sayyida Zainab mjini Cairo, Misri.
Habari ID: 3471372    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/26

TEHRAN (IQNA)-Arthur Wagner, mwanasiasa aliyekuwa chuki dhidi ya Uislamu amebadili msimamo ghafla na kutangaza kuwa amesilimu na hivyo kuukumbatia Uislamu katika maisha .
Habari ID: 3471370    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/24

TEHRAN (IQNA)-Waislamu nchini Marekani wamepanga kuswali mbele ya Ikulu White House mjini Washington DC na kisha kufanya maandamano makubwa ya kulalamikia ubaguzi wanaotendewa na utawala wa Rais Donald Trump.
Habari ID: 3471369    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/24

TEHRAN (IQNA)-Baraza la Waislamu Uingereza (MCB) limetangaza kuanzisha mpango mpya wa kukabiliana na ugaidi.
Habari ID: 3471366    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/22

TEHRAN (IQNA)-Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inapanga kuandaa mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya wanafunzi Waislamu katika mwezi wa Aprili sambamba na Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani ya Iran.
Habari ID: 3471365    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/22

TEHRAN (IQNA)-Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni Waislamu (IUMS) imelaani tawala za Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa kuendelea kuwashikilia kinyume cha sheria wahubiri wa Uislamu.
Habari ID: 3471362    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/20

IQNA (TEHRAN)-Serikali ya Bangladesh inasema wakimbizi Waislamu Warohingya waliopata hifadhi nchini kufuatia ukatili wanaotendewa nchini Myanmar sasa wamefika milioni moja na idadi hiyo ni kubwa zaidi ya ile ambayo imekuwa ikitajwa katika vyombo vya habari.
Habari ID: 3471360    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/19

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA) Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Marekani imekuwa ikifanya "ufidhuli mkubwa" kuhusu Quds Tukufu (Jerusalem) na kuongeza kuwa njama zake hizo hazitafika popote.
Habari ID: 3471357    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/17

TEHRAN (IQNA)-Mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini unatekeleza sera za kuwavutia watalii wa tamaduni na dini mbali mbali na kwa msingi huo kuna mpango maalumu wa kuwavutia watalii Waislamu katika fremu ya Utalii Halali.
Habari ID: 3471356    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/16

TEHRAN (IQNA)-Hafidh wa Qur'ani Tukufu kutoka Morocco ametangazwa mshindi katika Mashindano ya Tisa ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu nchini Sudan na kutunukiwa zawadi yake Jumamosi usiku.
Habari ID: 3471355    Tarehe ya kuchapishwa : 2018/01/15