Zaid al-Hameli alisema ujenzi na ukarabati wa misikiti ni moja ya shughuli kuu za jimuiya hiyo.
Alisema miradi ya ujenzi wa misikiti hiyo inafanywa katika nchi maskini ambazo watu wake wanahitaji maeneo zaidi ya ibada.
"Tunatumai kuigeuza misikiti hii ambayo imejengwa (na jumuiya) kuwa taa za kukuza (mafundisho ya Kiislamu), ufahamu na utamaduni," alisema.
Al-Hameli ameongeza kuwa, duru za Qur'ani, Iftar na matukio yanayosaidia kustawisha utamaduni wa Kiislamu ni miongoni mwa shughuli zinazofanywa katika misikiti hiyo.
Al-Najat Charity Society ni taasisi kuu ya kutoa misaada nchini Kuwait ambayo imekuza shughuli zake za Kurani na kidini katika miaka ya hivi karibuni.
Kufanya kozi za kufundisha Qur'ani mtandaoni kwa watoto na vijana na kuandaa programu za Qur'ani misikitini ni miongoni mwa shughuli zake.
4112138