TEHRAN (IQNA)- Rais Ebrahim Raisi amesema: taifa adhimu la Iran litatangaza kwa mara nyingine tena kwamba litabaki kuwa thabiti katika malengo ya Uislamu hadi itakapokombolewa Quds kikamilifu, kwa kushiriki kwa wingi katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds.

Seyed Ebrahim Raisi, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amehutubia hadhara ya waumini katika Haram ya Imam Khomeini (MA) kwa mnasaba wa mkesha wa tarehe 21 ya mwezi mtukufu wa Ramadhani iliyosadifiana na kumbukumbu ya kufa shahidi kiongozi wa wachamungu Amirul-Mu'minin Ali (AS), ambapo katika hotuba yake hiyo amesema, Imam Khomeini alilitangaza suala la Quds na Palestina kuwa kadhia muhimu zaidi kwa Ulimwengu wa Kiislamu na akaifanya Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kuwa Siku ya Kimataifa ya Quds na Siku ya kuwaunga mkono Wapalestina wanaodhulumiwa. Rais Raisi amesisitiza kwa kusema: "bila shaka yoyote katika siku ya 23 ya mwezi mtukufu wa Ramadhani itakayosadifiana na Siku ya Quds Duniani, taifa adhimu la Iran litashiriki kwa wingi katika maandamano na kutangaza kwamba litabaki kuwa thabiti katika malengo ya Uislamu hadi Quds itakapokombolewa kikamilifu".
4133533