IQNA

Muqawama (Mapambano ya Kiislamu)

Ijumaa ya 'Nasr', idadi kubwa ya waumini wajitokeza kumuenzi Sayyid wa Muqawama

12:18 - October 04, 2024
Habari ID: 3479531
IQNA-Khitma kwa ajili ya Mpigana Jihadi Katika Njia ya Allah, Sayyid Azizi wa Umma wa Kiislamu, Shahidi Hujjatul Islam wal Muslimin Sayyid Hassan Nasrallah na wenzake inafanyka katika kwa kaui mbiu ya 'Ijumaa ya Nasr" katika Uwanja wa Sala wa Imam Khomeini jijini Tehran.

Hafla hiyo ilianza rasmi saa nne unusu leo lakini watu kutoka mbali na karibu walifika kwenye sherehe hiyo kuanzia saa kumi na moja asubuhi na wakati  milango ya Uwanja wa Sala wa  Imam Khomeini (RA) ilifunguliwa kwa ajili ya kuwakakribisha waumini waliofika katika hafla ya Sayyid wa Muqawama (Sayyid Hassan Nasrallah). Waumini waliofika wamebainisha  kuchukizwa na jinai za kikatili za utawala mashuhuri wa Kizayuni huko Gaza na Lebanon.

Katika hafla hiyo inayofanyika kufuatia kuuawa shahidi mshika bendera ya muqawama na uhuru wa Quds na Palestina, Seyyed Hassan Nasrallah na Kiongozi wa Hamas Ismail Haniya pamoja na mashahidi wenzao, na katika mkesha wa kuadhimisha mwaka wa kwanza wa Operesheni ya Kimbunga cha Al- Aqsa ya wapiganaji wa harakati za muqawama (mapambano ya Kiislamu ya Palestina), Sala ya Ijumaa wiki hii mjini Tehran, Oktoba 4, itaswalishwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.

Hafla hiyo ya Khitma na Swala ya Ijumaa imeanza kwa usomaji wa aya za Qur’ani Tukufu na  Qari Mohammad Hossein Saidian.

Baadaye, Ahmed Babaei, mshairi mwanamapinduzi, alisoma mashairi ya kuomboleza kwa ajili ya Sayyid Hasan Nasrallah.

Baada ya hapo, Hossein Al-Akarf, msoma mashairi wa Bahrain, alisoma tungo za nafasi ya mujahid katika Njia ya Allah Allah, Sayyid Hassan Nasrallah.

Kisha, Haj Mehdi Rasuuli, mtunzaji wa Ahlul-Bayt (pbuh), akasoma mashairi yanayoelezea hadhi ya juu ya Shahidi Seyyed Hassan Nasrallah. Hafla hiyo imeendelea kwa kusomwa mashairi na aya za Qur’ani Tukufu kabla ya Kiongozi Muadhamu wa Mapindzi ya Kiislamu kuanza  hotuba za Swala  ya Ijumaa.

4240473

Habari zinazohusiana
captcha