IQNA

Mashindano ya Qur'ani

Washiriki 92 kutoka Nchi 71 wanahudhuria Mashindano ya 64 ya Kimataifa ya Qur’ani ya Malaysia  

21:35 - October 06, 2024
Habari ID: 3479548
IQNA – Mashindano ya 64 wa Kimataifa wa Kusoma na Kuhifadhi Qur'ani wa Malaysia yalifunguliwa rasmi Jumamosi, ambapo yana washiriki 92 kutoka nchi 71.

Sherehe ya ufunguzi ilifanyika katika Kituo cha Biashara cha Dunia huko Kuala Lumpur kwa kushirikisha washiriki, maafisa wa Malaysia, na umati wa watu.
Washiriki hao ni pamoja na maqari 53 na wahifadhi 39 wanaoshindana katika kategoria kadhaa.
Mashindano hayo, yenye mada Al-Falah yataendelea hadi Oktoba 12.
Sherehe ya ufunguzi ilijumuisha somo la msomaji bingwa mara tano wa Malaysia Rahmas Abdullah na qasida ya Kikosi cha Kidini cha Jeshi la Wanajeshi la Malaysia (Kagat).
Akihutubia sherehe za ufunguzi, Waziri Mkuu wa Malaysia Anwar Ibrahim alisisitiza umuhimu wa umoja na hekima.
"Fikra finyu zitatuzamisha. Wakati huohuo, mawazo yasiyo na busara yatakuwa changamoto kwetu," alisema.
Alisisitiza haja ya uelewa, subira, na hekima katika kufanya maamuzi, hasa kwa kuzingatia vita vinavyoendelea vya Israel dhidi ya Gaza.
Mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya Malaysia kila mwaka huandaliwa katika mji mkuu wa nchi hiyo wa Kuala Lumpur na Idara ya Maendeleo ya Kiislamu ya nchi hiyo (JAKIM).

3490157

Habari zinazohusiana
captcha