Kikiwa kwenye Barabara ya Brant chini ya mnara wa maji wa Alief, kituo hicho kinalenga kukuza uelewa wa kina wa uhusiano wa kihistoria na kitamaduni kati ya Uislamu na jamii zinazozungumza Kihispania.
Waislamu wanaozungumza Kihispania sio wengi, haswa huko Houston. Hata hivyo, kituo hicho cha Centro Islámico kinalenga kuleta mwonekano mkubwa zaidi kwa jumuiya hii, ikitoa nyenzo na suhula za elimu ili kusaidia safari zao za kiroho.
Mwanzilishi mwenza Jaime "Mujahid" Fletcher alionyesha dhamira pana ya kituo hicho katika taarifa. "Kituo cha IslamInSpanish Centro Islámico kinawakilisha zaidi ya jengo-ni utimilifu wa maono ya kubadilisha maisha. Ingawa sauti zetu zimesikika kwenye vyombo vya habari vya kawaida kitaifa na kimataifa, lengo letu siku zote limekuwa kuona maisha yakibadilishwa kuwa raia wa kimataifa wenye tija wakishirikiana kwa manufaa ya binadamu wote.”
3490699