IQNA

Msikiti nchini Uingereza wapongezwa kwa kukusanya tani 120 za taka 

20:46 - April 12, 2025
Habari ID: 3480530
IQNA-Msikiti wa UKIM Sparkbrook Islamic Centre huko Birmingham, Uingereza, umesifiwa kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Birmingham kukusanya tani 120 za taka.

Siku ya Alhamisi, Aprili 3, kiasi kikubwa cha takataka zilizotupwa kiholela zilitolewa kwenye kituo cha jamii cha Tyseley. Msikiti uliitisha mkutano ili kupanga mpango wa kukabiliana na hali hiyo. Siku ya Jumamosi, Aprili 5, watu 40 walikusanyika mapema wakisubiri magari ya taka. Haraka waligawanywa kwenye maeneo mawili kusaidia katika shughuli hiyo

Diwani  Mahmood wa baraza la jiji alisifu juhudi za jamii: "Hii ni mfano mzuri wa ushirikiano tunaojenga na vikundi vya jamii kusaidia kuweka jiji letu safi." Alishukuru mwenyekiti Mohammed Ishtiaq na wanajamii waliojitolea kwa msaada wao.

Birmingham inakumbwa na changamoto kubwa ya taka kutokana na mgomo unaoendelea wa wafanyakazi wa ukusanyaji taka. Mgomo huu ulitokana na mzozo kuhusu kupunguzwa kwa mishahara na kuondolewa kwa baadhi ya nafasi za kazi. Kutokusanywa kwa taka kumesababisha hofu ya kiafya, ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa panya wakubwa na harufu mbaya. Wakazi na viongozi wa mitaa wanashinikiza suluhisho ili kurejesha usafi na kuondoa hatari zinazoongezeka za kiafya.

349265

captcha