IQNA

Waziri Mkuu wa Malaysia ahudhuria Mashindano ya Kitaifa ya Qur'ani 

21:49 - April 28, 2025
Habari ID: 3480604
IQNA – Waziri Mkuu wa Malaysia, Anwar Ibrahim, alifungua rasmi Mashindano ya Kitaifa ya Kusoma na Kuhifadhi Qur'ani kwa mwaka 1446H/2025. 

Mashindano hayo yalianza Jumapili huko Kangar, Jimbo la Perlis, yakihusisha washiriki 109. Litaendelea hadi Mei 2, 2025. 

Akihutubia hafla hiyo, Anwar amesema kuwa nchi inapaswa kuendelea kwa nguvu na maendeleo kwa msingi wa maadili na mafunzo. 

"Ni kweli, kuna haja, nchi lazima iendelee kwa nguvu na maendeleo, haipaswi kuachwa nyuma katika sekta yoyote, lakini maendeleo yetu lazima yawe kwa msingi wa maadili na mafunzo, na hili linatutofautisha na mitazamo na itikadi nyingine. 

"... na kwa ulafi unaotokea, hasa katika dunia ya leo, unapinga kanuni nzima za maadili ya kibinadamu," amesema katika hotuba yake. 

Anwar pia amesema kuwa kufahamu Qur'ani ni msingi wa kuinua heshima na maendeleo ya Waislamu nchini kuelekea kujenga ustaarabu na taifa la Madani. 

Wakati huo huo, amesisitiza kuwa ujuzi wa lugha, teknolojia ya kidijitali na Akili Mnemba (AI) pia unapaswa kupewa kipaumbele ili kuzuia Waislamu wasiachwe nyuma katika maeneo haya. 

"Ningependa kuwakumbusha na kuwasihi marafiki zangu wenye uwezo wa kufundisha, kumbukeni kuwa changamoto zetu ni ngumu sana na Waislamu wanahitaji kufanya kitu kipya, chenye nguvu, na cha ujasiri zaidi," alisema.

3492857

Habari zinazohusiana
Kishikizo: qurani tukufu malaysia
captcha