
Kwa mujibu wa taarifa, walioshiriki ziara hiyo ni miongoni mwa washiriki wa kozi iitwayo “Maandalizi ya Walinganiaji wa Kisasa”.
Kozi hiyo hudumu kwa miezi miwili, na mara hii imewaleta pamoja washiriki kutoka Algeria, Nigeria, India, Ghana, Togo, Bangladesh na Madagascar.
Sheikh Hassan Al-Sagheer, rais wa Chuo cha Kimataifa cha Al-Azhar , alisema ziara hii ni sehemu ya programu pana inayotekelezwa na chuo hicho kwa lengo la kuwafahamisha washiriki kuhusu maeneo ya kidini na kitamaduni nchini Misri.
Akirejea ziara atika Msikiti Mkuu wa Al-Azhar wiki iliyopita, aliongeza kuwa: “Washiriki wa ziara hii walitambulishwa historia tajiri na nyua za msikiti huu, pamoja na nafasi yake katika kueneza na kupanua elimu za Kiislamu na lugha ya Kiarabu, na kuimarisha msimamo wa wastani (wasatiyya).”
Al-Sagheer pia alisema kuwa utofauti wa ziara hizi unaakisi mtazamo wa Al-Azhar wa kulea wahubiri wenye uelewa wa maarifa ya kidini na kitamaduni. Ziara hizo zinawasaidia kuwafahamisha urithi mpana wa Misri wa kitamaduni, kihistoria na kibinadamu, na kuongeza uwezo wao wa kuwasilisha taswira sahihi ya ujumbe wa Al-Azhar duniani kote.
Programu hiyo ilijumuisha kutembelea alama kadhaa muhimu za kihistoria na kidini katika eneo la Fustat, ambapo Mohammed Al-Jazeeri, mhadhiri katika Idara ya Ustaarabu wa Kiislamu ya Kitivo cha Lugha ya Kiarabu cha Al-Azhar, alitoa maelezo ya kina kuhusu historia na umuhimu wa kitamaduni wa eneo hilo. Alisisitiza thamani ya kihistoria ya Msikiti Mkuu wa Amr ibn Al-As na nafasi yake muhimu katika harakati za kielimu na dawah katika nyakati tofauti.
Ziara hiyo pia ilihusisha kutembelea vivutio kadhaa maarufu vya Kikristo, vikiwemo Kanisa la Hanging (Al-Mu‘allaqa) na Kanisa la Abi Serje, ambako washiriki walijifunza kuhusu umuhimu wa kihistoria wa maeneo hayo.
Vilevile, walinganiaji hao wageni walitembelea Ngome ya Bablyon, miongoni mwa maeneo ya kale zaidi ya akiolojia nchini Misri, inayotoa taswira ya vipindi vya kihistoria kuanzia zama za Warumi hadi zama za Uislamu.
4355536